< Zaburi 78 >

1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
Cantico di Asaf. Ascolta, popolo mio, il mio insegnamento; porgete gli orecchi alle parole della mia bocca!
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
Io aprirò la mia bocca per proferir parabole, esporrò i misteri de’ tempi antichi.
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
Quel che noi abbiamo udito e conosciuto, e che i nostri padri ci hanno raccontato,
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
non lo celeremo ai loro figliuoli; diremo alla generazione avvenire le lodi dell’Eterno, e la sua potenza e le maraviglie ch’egli ha operato.
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
Egli stabilì una testimonianza in Giacobbe, e pose una legge in Israele, ch’egli ordinò ai nostri padri di far conoscere ai loro figliuoli,
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
perché fossero note alla generazione avvenire, ai figliuoli che nascerebbero, i quali alla loro volta le narrerebbero ai loro figliuoli,
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
ond’essi ponessero in Dio la loro speranza e non dimenticassero le opere di Dio, ma osservassero i suoi comandamenti;
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
e non fossero come i loro padri, una generazione caparbia e ribelle, una generazione dal cuore incostante, e il cui spirito non fu fedele a Dio.
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
I figliuoli di Efraim, gente di guerra, buoni arcieri, voltaron le spalle il dì della battaglia.
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
Non osservarono il patto di Dio, e ricusarono di camminar secondo la sua legge;
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
e dimenticarono le sue opere e i prodigi ch’egli avea loro fatto vedere.
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
Egli avea compiuto maraviglie in presenza de’ loro padri, nel paese d’Egitto, nelle campagne di Zoan.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
Fendé il mare e li fece passare, e fermò le acque come in un mucchio.
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
Di giorno li guidò con una nuvola, e tutta la notte con una luce di fuoco.
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
Schiantò rupi nel deserto, e li abbeverò copiosamente, come da gorghi.
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
Fece scaturire ruscelli dalla roccia e ne fece scender dell’acque a guisa di fiumi.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
Ma essi continuarono a peccare contro di lui, a ribellarsi contro l’Altissimo, nel deserto;
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
e tentarono Dio in cuor loro, chiedendo cibo a lor voglia.
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
E parlarono contro Dio, dicendo: Potrebbe Dio imbandirci una mensa nel deserto?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
Ecco, egli percosse la roccia e ne colarono acque, ne traboccaron torrenti; potrebb’egli darci anche del pane, e provveder di carne il suo popolo?
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
Perciò l’Eterno, avendoli uditi, s’adirò fieramente, e un fuoco s’accese contro Giacobbe, e l’ira sua si levò contro Israele,
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
perché non aveano creduto in Dio, né avevano avuto fiducia nella sua salvazione;
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
eppure egli comandò alle nuvole di sopra, e aprì le porte del cielo,
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
e fece piover su loro manna da mangiare, e dette loro del frumento del cielo.
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
L’uomo mangiò del pane dei potenti; egli mandò loro del cibo a sazietà.
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
Fece levare in cielo il vento orientale, e con la sua potenza addusse il vento di mezzodì;
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
fece piover su loro della carne come polvere, degli uccelli alati, numerosi come la rena del mare;
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
e li fece cadere in mezzo al loro campo, d’intorno alle loro tende.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
Così essi mangiarono e furon ben satollati, e Dio mandò loro quel che aveano bramato.
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
Non si erano ancora distolti dalle loro brame, avevano ancora il loro cibo in bocca,
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
quando l’ira di Dio si levò contro loro, e ne uccise tra i più fiorenti, e abbatté i giovani d’Israele.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
Con tutto ciò peccarono ancora, e non credettero alle sue maraviglie.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
Ond’egli consumò i loro giorni in vanità, e i loro anni in ispaventi.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
Quand’ei li uccideva, essi lo ricercavano e tornavano bramosi di ritrovare Iddio;
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
e si ricordavano che Dio era la loro ròcca, l’Iddio altissimo il loro redentore.
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
Essi però lo lusingavano con la loro bocca, e gli mentivano con la loro lingua.
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
Il loro cuore non era diritto verso lui, e non eran fedeli al suo patto.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
Ma egli, che è pietoso, che perdona l’iniquità e non distrugge il peccatore, più volte rattenne la sua ira, e non lasciò divampare tutto il suo cruccio.
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
Ei si ricordò ch’essi erano carne, un fiato che passa e non ritorna.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
Quante volte si ribellarono a lui nel deserto, e lo contristarono nella solitudine!
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
E tornarono a tentare Iddio e a provocare il Santo d’Israele.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
Non si ricordaron più della sua mano, del giorno in cui egli li liberò dal nemico,
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
quando operò i suoi miracoli in Egitto, e i suoi prodigi nelle campagne di Zoan;
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
mutò i loro fiumi in sangue, e i loro rivi in guisa che non potean più bere;
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
mandò contro loro mosche velenose che li divoravano, e rane che li distruggevano;
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
dette il loro raccolto ai bruchi e la loro fatica alle locuste;
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
distrusse le loro vigne con la gragnuola e i loro sicomori coi grossi chicchi d’essa;
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
abbandonò il loro bestiame alla grandine e le lor gregge ai fulmini.
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
Scatenò su loro l’ardore del suo cruccio, ira, indignazione e distretta, una torma di messaggeri di malanni.
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
Dette libero corso alla sua ira; non preservò dalla morte la loro anima, ma abbandonò la loro vita alla pestilenza.
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
Percosse tutti i primogeniti d’Egitto, le primizie del vigore nelle tende di Cham;
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
ma fece partire il suo popolo a guisa di pecore, e lo condusse a traverso il deserto come una mandra.
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
Lo guidò sicuramente sì che non ebbero da spaventarsi, mentre il mare inghiottiva i loro nemici.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
Li fece arrivare alla sua santa frontiera, alla montagna che la sua destra avea conquistato.
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
Scacciò le nazioni dinanzi a loro, ne assegnò loro a sorte il paese quale eredità, e nelle tende d’esse fece abitare le tribù d’Israele.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
E nondimeno tentarono l’Iddio altissimo e si ribellarono e non osservarono le sue testimonianze.
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
Si trassero indietro e furono sleali come i loro padri; si rivoltarono come un arco fallace;
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
lo provocarono ad ira coi loro alti luoghi, lo mossero a gelosia con le loro sculture.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
Dio udì questo, e si adirò, prese Israele in grande avversione,
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
onde abbandonò il tabernacolo di Silo, la tenda ov’era dimorato fra gli uomini;
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
e lasciò menare la sua Forza in cattività, e lasciò cader la sua Gloria in man del nemico.
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
Abbandonò il suo popolo alla spada, e s’adirò contro la sua eredità.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
Il fuoco consumo i loro giovani, e le loro vergini non ebber canto nuziale.
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
I loro sacerdoti caddero per la spada, e le loro vedove non fecer lamento.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
Poi il Signore si risvegliò come uno che dormisse, come un prode che grida eccitato dal vino.
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
E percosse i suoi nemici alle spalle, e mise loro addosso un eterno vituperio.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
Ma ripudiò la tenda di Giuseppe, e non elesse la tribù di Efraim;
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
ma elesse la tribù di Giuda, il monte di Sion ch’egli amava.
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
Edificò il suo santuario a guisa de’ luoghi eccelsi, come la terra ch’egli ha fondata per sempre.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
Elesse Davide, suo servitore, lo prese dagli ovili;
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
lo trasse di dietro alle pecore lattanti, per pascere Giacobbe suo popolo, ed Israele sua eredità.
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
Ed egli li pasturò secondo l’integrità del suo cuore, e li guidò con mano assennata.

< Zaburi 78 >