< Zaburi 78 >

1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
משכיל לאסף האזינה עמי תורתי הטו אזנכם לאמרי פי׃
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
אפתחה במשל פי אביעה חידות מני קדם׃
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
אשר שמענו ונדעם ואבותינו ספרו לנו׃
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
לא נכחד מבניהם לדור אחרון מספרים תהלות יהוה ועזוזו ונפלאותיו אשר עשה׃
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
ויקם עדות ביעקב ותורה שם בישראל אשר צוה את אבותינו להודיעם לבניהם׃
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
למען ידעו דור אחרון בנים יולדו יקמו ויספרו לבניהם׃
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
וישימו באלהים כסלם ולא ישכחו מעללי אל ומצותיו ינצרו׃
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
ולא יהיו כאבותם דור סורר ומרה דור לא הכין לבו ולא נאמנה את אל רוחו׃
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
בני אפרים נושקי רומי קשת הפכו ביום קרב׃
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
לא שמרו ברית אלהים ובתורתו מאנו ללכת׃
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
וישכחו עלילותיו ונפלאותיו אשר הראם׃
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
נגד אבותם עשה פלא בארץ מצרים שדה צען׃
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
בקע ים ויעבירם ויצב מים כמו נד׃
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
וינחם בענן יומם וכל הלילה באור אש׃
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
יבקע צרים במדבר וישק כתהמות רבה׃
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
ויוצא נוזלים מסלע ויורד כנהרות מים׃
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
ויוסיפו עוד לחטא לו למרות עליון בציה׃
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
וינסו אל בלבבם לשאל אכל לנפשם׃
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
וידברו באלהים אמרו היוכל אל לערך שלחן במדבר׃
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
הן הכה צור ויזובו מים ונחלים ישטפו הגם לחם יוכל תת אם יכין שאר לעמו׃
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
לכן שמע יהוה ויתעבר ואש נשקה ביעקב וגם אף עלה בישראל׃
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
כי לא האמינו באלהים ולא בטחו בישועתו׃
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
ויצו שחקים ממעל ודלתי שמים פתח׃
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
וימטר עליהם מן לאכל ודגן שמים נתן למו׃
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
לחם אבירים אכל איש צידה שלח להם לשבע׃
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
יסע קדים בשמים וינהג בעזו תימן׃
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
וימטר עליהם כעפר שאר וכחול ימים עוף כנף׃
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
ויפל בקרב מחנהו סביב למשכנתיו׃
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
ויאכלו וישבעו מאד ותאותם יבא להם׃
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
לא זרו מתאותם עוד אכלם בפיהם׃
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
ואף אלהים עלה בהם ויהרג במשמניהם ובחורי ישראל הכריע׃
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
בכל זאת חטאו עוד ולא האמינו בנפלאותיו׃
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
ויכל בהבל ימיהם ושנותם בבהלה׃
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
אם הרגם ודרשוהו ושבו ושחרו אל׃
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
ויזכרו כי אלהים צורם ואל עליון גאלם׃
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
ויפתוהו בפיהם ובלשונם יכזבו לו׃
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
ולבם לא נכון עמו ולא נאמנו בבריתו׃
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
והוא רחום יכפר עון ולא ישחית והרבה להשיב אפו ולא יעיר כל חמתו׃
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
ויזכר כי בשר המה רוח הולך ולא ישוב׃
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
כמה ימרוהו במדבר יעציבוהו בישימון׃
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
וישובו וינסו אל וקדוש ישראל התוו׃
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
לא זכרו את ידו יום אשר פדם מני צר׃
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
אשר שם במצרים אתותיו ומופתיו בשדה צען׃
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
ויהפך לדם יאריהם ונזליהם בל ישתיון׃
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
ישלח בהם ערב ויאכלם וצפרדע ותשחיתם׃
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
ויתן לחסיל יבולם ויגיעם לארבה׃
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
יהרג בברד גפנם ושקמותם בחנמל׃
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
ויסגר לברד בעירם ומקניהם לרשפים׃
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
ישלח בם חרון אפו עברה וזעם וצרה משלחת מלאכי רעים׃
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
יפלס נתיב לאפו לא חשך ממות נפשם וחיתם לדבר הסגיר׃
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
ויך כל בכור במצרים ראשית אונים באהלי חם׃
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
ויסע כצאן עמו וינהגם כעדר במדבר׃
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
וינחם לבטח ולא פחדו ואת אויביהם כסה הים׃
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
ויביאם אל גבול קדשו הר זה קנתה ימינו׃
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
ויגרש מפניהם גוים ויפילם בחבל נחלה וישכן באהליהם שבטי ישראל׃
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
וינסו וימרו את אלהים עליון ועדותיו לא שמרו׃
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
ויסגו ויבגדו כאבותם נהפכו כקשת רמיה׃
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
ויכעיסוהו בבמותם ובפסיליהם יקניאוהו׃
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
שמע אלהים ויתעבר וימאס מאד בישראל׃
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
ויטש משכן שלו אהל שכן באדם׃
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
ויתן לשבי עזו ותפארתו ביד צר׃
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
ויסגר לחרב עמו ובנחלתו התעבר׃
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
בחוריו אכלה אש ובתולתיו לא הוללו׃
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
כהניו בחרב נפלו ואלמנתיו לא תבכינה׃
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
ויקץ כישן אדני כגבור מתרונן מיין׃
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
ויך צריו אחור חרפת עולם נתן למו׃
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
וימאס באהל יוסף ובשבט אפרים לא בחר׃
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
ויבחר את שבט יהודה את הר ציון אשר אהב׃
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
ויבן כמו רמים מקדשו כארץ יסדה לעולם׃
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
ויבחר בדוד עבדו ויקחהו ממכלאת צאן׃
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
מאחר עלות הביאו לרעות ביעקב עמו ובישראל נחלתו׃
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
וירעם כתם לבבו ובתבונות כפיו ינחם׃

< Zaburi 78 >