< Zaburi 78 >

1 Watu wangu, sikieni mafundisho yangu, sikilizeni maneno ya kinywa changu.
The lernyng of Asaph. Mi puple, perseyue ye my lawe; bowe youre eere in to the wordis of my mouth.
2 Nitafungua kinywa changu katika mifano; nitaimba kuhusu mambo yaliyofichika yahusuyo yaliyopita.
I schal opene my mouth in parablis; Y schal speke perfite resouns fro the bigynnyng.
3 Haya ni mambo ambayo tumeyasikia na kujifunza mambo ambayo mababu zetu wametuambia sisi. Hatutawaficha uzao wao.
Hou grete thingis han we herd, aud we han knowe tho; and oure fadris. telden to vs.
4 Tutawaambia kizazi kijacho kuhusu sifa anazostahili Yahwe kwa matendo yake, nguvu zake, na maajabu ambayo ameyafanya.
Tho ben not hid fro the sones of hem; in anothir generacioun. And thei telden the heriyngis of the Lord, and the vertues of hym; and hise merueilis, whyche he dide.
5 Kwa kuwa yeye alianzisha agano la amri katika Yakobo na sheria maalumu katika Israeli. Yeye aliamuru mababu zetu kuwa walipaswa kuzifundisha kwa watoto wao.
And he reiside witnessyng in Jacob; and he settide lawe in Israel. Hou grete thingis comaundide he to oure fadris, to make tho knowun to her sones;
6 Aliamuru hivi ili kwamba kizazi kijacho kiweze kuzijua amri zake, ili wawafundishe wana ambao bado hawajazaliwa.
that another generacioun knowe. Sones, that schulen be born, and schulen rise vp; schulen telle out to her sones.
7 Kisha wangeweka tumaini lao katika Mungu na kutokusahau matendo yake bali wazishike amri zake.
That thei sette her hope in God, and foryete not the werkis of God; and that thei seke hise comaundementis.
8 Ndipo wasingekuwa kama mababu zao, ambao walikuwa wakaidi na wenye uasi, kizazi ambacho mioyo yao haikuwa kamilifu, na ambao roho zao hazikuwa na nia thabiti na aminifu kwa Mungu.
Lest thei be maad a schrewid generacioun; and terrynge to wraththe, as the fadris of hem. A generacioun that dresside not his herte; and his spirit was not bileued with God.
9 Waefraimu walikuwa na silaha na upinde, lakini walikimbia siku ya vita.
The sones of Effraym, bendinge a bouwe and sendynge arowis; weren turned in the dai of batel.
10 Hawakutunza agano na Mungu, na walikataa kutii sheria yake.
Thei kepten not the testament of God; and thei nolden go in his lawe.
11 Walisahau matendo yake, mambo ya ajabu ambayo yeye amewaonesha wao.
And thei foryaten hise benefices; and hise merueils, whiche he schewide to hem.
12 Walisahau mambo ya ajabu aliyofayafanya machoni pa mababu zao katika nchi ya Misri, katika ardhi ya Soani.
He dide merueils bifore the fadris of hem in the loond of Egipt; in the feeld of Taphneos.
13 Aliigawa bahari na akawaongoza katikati ya bahari; aliyafanya maji yasimame kama kuta.
He brak the see, and ledde hem thorou; and he ordeynede the watris as in a bouge.
14 Wakati wa mchana aliwaongoza kwa wingu na usiku wote kwa nuru ya moto.
And he ledde hem forth in a cloude of the dai; and al niyt in the liytnyng of fier.
15 Alipasua miamba jangwani, na aliwapa maji mengi, ya kutosha kujaza vina virefu vya bahari.
He brak a stoon in deseert; and he yaf watir to hem as in a myche depthe.
16 Alifanya maporomoko ya maji kutiririka tokea mwambani na aliyafanya maji yatiririke kama mito.
And he ledde watir out of the stoon; and he ledde forth watris as floodis.
17 Lakini bado waliendelea kutenda dhambi dhidi yake, wakiasi dhidi ya Aliye Juu katika jangwa.
And thei `leiden to yit to do synne ayens hym; thei excitiden hiye God in to ire, in a place with out water.
18 Walimjaribu Mungu mioyoni mwao kwa kuomba chakula cha kuwatosheleza hamu zao.
And thei temptiden God in her hertis; that thei axiden meetis to her lyues.
19 Waliongea dhidi ya Mungu; walisema, “Kweli Mungu anaweza kuweka meza ya chakula kwa ajili yetu jangwani?
And thei spaken yuel of God; thei seiden, Whether God may make redi a bord in desert?
20 Tazama, wakati alipoupiga mwamba, maji yalibubujika, mito ikafurika. Lakini anaweza kutoa mkate tena? Ataweza kuleta nyama kwa watu wake?”
For he smoot a stoon, and watris flowiden; and streemys yeden out in aboundaunce. Whether also he may yyue breed; ether make redi a bord to his puple?
21 Yahwe aliposikia haya, alikasirika; moto wake uliwaka dhidi ya Yakobo, hasira yake ikamshambulia Israeli,
Therfor the Lord herde, and delaiede; and fier was kindelid in Jacob, and the ire of God stiede on Israel.
22 kwa sababu hawakumwamini Mungu na hawakuamini katika wokovu wake.
For thei bileueden not in God; nether hopiden in his heelthe.
23 Lakini yeye bado aliziamuru mbingu juu na kufungua milango ya mbingu.
And he comaundide to the cloudis aboue; and he openyde the yatis of heuene.
24 Aliwanyeshea mana ili wale, na aliwapa nafaka kutoka mbinguni.
And he reynede to hem manna for to eete; and he yaf to hem breed of heuene.
25 Watu walikula mikate ya malaika. Aliwatumia chakula kingi.
Man eet the breed of aungels; he sent to hem meetis in aboundance.
26 Alisababisha upepo wa mashariki kupiga mawinguni, na kwa uweza wake aliuongoza upepo wa kusini.
He turnede ouere the south wynde fro heuene; and he brouyte in bi his vertu the weste wynde.
27 Aliwanyeshea nyama kama mavumbi, na ndege kama wingi wa mchanga wa baharini.
And he reynede fleischis as dust on hem; and `he reinede volatils fethered, as the grauel of the see.
28 Walianguka katikati ya kambi yao, na maeneo yote karibu na hema zao.
And tho felden doun in the myddis of her castels; aboute the tabernaclis of hem.
29 Hivyo walikula na walishiba. Maana aliwapa kile walichokitamani sana.
And thei eeten, and weren fillid greetli, and he brouyte her desire to hem;
30 Lakini walikuwa bado hawajatosheka; chakula chao kilikuwa bado kinywani mwao.
thei weren not defraudid of her desier. Yit her metis weren in her mouth;
31 Ndipo hasira ya Mungu iliwashambulia na kuwaua wenye nguvu kati yao. Aliwaangusha chini vijana wa Israeli.
and the ire of God stiede on hem. And he killide the fatte men of hem; and he lettide the chosene men of Israel.
32 Licha ya hili, waliendelea kutenda dhambi na hawakuyaamini matendo yake ya ajabu.
In alle these thingis thei synneden yit; and bileuede not in the merueils of God.
33 Hivyo Mungu alizikatisha siku zao; miaka yao ilijawa na hofu.
And the daies of hem failiden in vanytee; and the yeeris of hem faileden with haste.
34 Wakati wowote Mungu alipowataabisha, nao waligeuka na kumtafuta yeye kwa bidii.
Whanne he killide hem, thei souyten hym; and turneden ayen, and eerli thei camen to hym.
35 Walikumbuka kuwa Mungu alikuwa mwamba wao na kuwa Mungu Aliye Juu Sana alikuwa mwokozi wao.
And thei bithouyten, that God is the helper of hem; and `the hiy God is the ayenbier of hem.
36 Lakini walimsifia tu kwa vinywa vyao na kumdanganya kwa maneno yao.
And thei loueden hym in her mouth; and with her tunge thei lieden to hym.
37 Maana mioyo yao haikuwa thabiti kwake, na hawakuwa waaminifu kwa agano lake.
Forsothe the herte of hem was not riytful with hym; nethir thei weren had feithful in his testament.
38 Lakini yeye, kwa kuwa alikuwa alikuwa na huruma, aliwasamehe uovu wao na hakuwaangamiza. Ndiyo, wakati mwingi aliizuia hasira yake na hakuionesha ghadhabu yake yote.
But he is merciful, and he schal be maad merciful to the synnes of hem; and he schal not destrie hem. And he dide greetli, to turne awei his yre; and he kyndelide not al his ire.
39 Alikumbuka kuwa waliumbwa kwa mwili, upepo ambao hupita nao haurudi.
And he bithouyte, that thei ben fleische; a spirit goynge, and not turnynge ayen.
40 Mara ngapi wameasi dhidi yake jangwani na kumuhuzunisha nyikani!
Hou oft maden thei hym wrooth in desert; thei stireden hym in to ire in a place with out watir.
41 Tena na tena walimjaribu Mungu na wakamtilia mashaka Mtakatifu wa Israeli.
And thei weren turned, and temptiden God; and thei wraththiden the hooli of Israel.
42 Hawakufikiria kuhusu uweza wake, jinsi alivyo waokoa dhidi ya adui
Thei bithouyten not on his hond; in the dai in the which he ayen bouyte hem fro the hond of the trobler.
43 alipofanya ishara za kutisha katika Misri na maajabu yake katika konde la Soani.
As he settide hise signes in Egipt; and hise grete wondris in the feeld of Taphneos.
44 Aligeuza mito ya Wamisri kuwa damu ili wasipate kunywa kutoka katika vijito vyao.
And he turnede the flodis of hem and the reynes of hem in to blood; that thei schulden not drynke.
45 Alituma makundi ya inzi yaliyowavamia na vyura ambao walisambaa katika nchi yao.
He sente a fleisch flie in to hem, and it eet hem; and he sente a paddok, and it loste hem.
46 Aliwapa mazao yao panzi na kazi yao nzige.
And he yaf the fruytis of hem to rust; and he yaf the trauels of hem to locustis.
47 Aliiharibu mizabibu yao kwa mvua ya mawe na miti ya mikuyu kwa mvua ya mawe zaidi.
And he killide the vynes of hem bi hail; and the moore trees of hem bi a frost.
48 Aliinyeshea mifugo yao mvua ya mawe na alirusha radi ya umeme ikapiga mifugo yao. Ukali wa hasira yake ulielekea dhidi yao.
And he bitook the beestis of hem to hail; and the possessioun of hem to fier.
49 Alituma gadhabu, uchungu na taabu kama wakala aletaye maafa.
He sente in to hem the ire of his indignacioun; indignacioun, and ire, and tribulacioun, sendingis in bi iuel aungels.
50 Aliifanyia njia hasira yake; hakuwakinga dhidi ya kifo bali aliwakabidhi kwa pigo.
He made weie to the path of his ire, and he sparide not fro the deth of her lyues; and he closide togidere in deth the beestis of hem.
51 Aliwaua wazaliwa wote wa kwanza katika Misri, wazaliwa wa kwanza wa nguvu zao katika mahema ya Hamu.
And he smoot al the first gendrid thing in the lond of Egipt; the first fruytis of alle the trauel of hem in the tabernaclis of Cham.
52 Aliwaongoza nje watu wake mwenyewe kama kondoo na aliwaelekeza kupitia jangwani kama kundi.
And he took awei his puple as scheep; and he ledde hem forth as a flok in desert.
53 Aliwaongoza salama na pasipo na woga, lakini bahari iliwaelemea adui zao.
And he ledde hem forth in hope, and thei dredden not; and the see hilide the enemyes of hem.
54 Kisha aliwaleta mpaka wa nchi yake takatifu, kwenye mlima huu ambao aliutwaa kwa mkono wake wa kuume.
And he brouyte hem in to the hil of his halewyng; in to the hil which his riythond gat. And he castide out hethene men fro the face of hem; and bi lot he departide to hem the lond in a cord of delyng.
55 Aliwafukuza mataifa mbele yao na akawapa urithi wao. Aliwakalisha makabila ya Israeli katika mahema yao.
And he made the lynagis of Israel to dwelle in the tabernaclis of hem.
56 Lakini bado walimjaribu na walimkaidi Mungu Aliye Juu na hawakushika amri zake takatifu.
And thei temptiden, and wraththiden heiy God; and thei kepten not hise witnessyngis.
57 Hawakuwa waaminifu na walienenda katika hila kama baba zao; walikuwa sio wa kutegemewa kama upinde mbovu.
And thei turneden awei hem silf, and thei kepten not couenaunt; as her fadris weren turned in to a schrewid bouwe.
58 Kwa maana walimkasirisha kwa mahali pao pa juu na walimgadhabisha hata akawa na hasira ya wivu kwa miungu yao.
Thei stiriden him in to ire in her litle hillis; and thei terriden hym to indignacioun of her grauen ymagis.
59 Mungu aliposikia hili, alikasirika na alimkataa kabisa Israeli.
God herde, and forsook; and brouyte to nouyt Israel greetli.
60 Alipaacha patakatifu pa Shilo, na hema alikoishi kati ya watu.
And he puttide awei the tabernacle of Sylo; his tabernacle where he dwellide among men.
61 Aliruhusu nguvu zake kutekwa na kuutoa utukufu wake mkononi mwa adui.
And he bitook the vertu of hem in to caitiftee; and the fairnesse of hem in to the hondis of the enemye.
62 Aliukabidhi upanga watu wake, na aliukasirikia urithi wake.
And he closide togidere his puple in swerd; and he dispiside his erytage.
63 Moto uliwavamia vijana wao wa kiume, na vijana wao wa kike hawakuwa na nyimbo za harusi.
Fier eet the yonge men of hem; and the virgyns of hem weren not biweilid.
64 Makuhani wao waliangushwa kwa upanga, na wajane wao hawakulia.
The prestis of hem fellen doun bi swerd; and the widewis of hem weren not biwept.
65 Kisha Bwana aliamshwa kama aliyetoka usingizini, kama shujaa apigaye kelele kwa sababu ya mvinyo.
And the Lord was reisid, as slepynge; as miyti greetli fillid of wiyn.
66 Aliwarudisha adui zake nyuma; aliwaweka kwenye aibu ya milele.
And he smoot hise enemyes on the hynderere partis; he yaf to hem euerlastyng schenschipe.
67 Aliikataa hema ya Yusufu, na hakulichagua kabila la Efraimu.
And he puttide awei the tabernacle of Joseph; and he chees not the lynage of Effraym.
68 Alilichagua kabila la Yuda na Mlima Sayuni aliyoupenda.
But he chees the lynage of Juda; he chees the hil of Syon, which he louede.
69 Alipajenga patakatifu pake kama mbinguni, na kama nchi aliyoiimarisha milele.
And he as an vnicorn bildide his hooli place; in the lond, which he foundide in to worldis.
70 Alimchagua Daudi, mtumishi wake, alimchukua kutoka zizi la kondoo.
And he chees Dauid his seruaunt, and took hym vp fro the flockis of scheep; he took hym fro bihynde scheep with lambren.
71 Alimtoa kutoka katika kufuata kondoo pamoja na wana wao, na kumweka kuwa mchungaji wa Yakobo, watu wake, na Israeli, urithi wake.
To feed Jacob his seruaunt; and Israel his eritage.
72 Daudi aliwachunga kwa uadilifu wa moyo wake, naye aliwaongoza kwa ujuzi wa mikono yake.
And he fedde hem in the innocens of his herte; and he ledde hem forth in the vndurstondyngis of his hondis.

< Zaburi 78 >