< Zaburi 77 >

1 Nitampazia Mungu sauti yangu, nitamuita Mungu kwa sauti yangu, na Mungu wangu atanisikia.
For the Leader; for Jeduthun. A Psalm of Asaph. I will lift up my voice unto God, and cry; I will lift up my voice unto God, that He may give ear unto me.
2 Katika siku ya taabu nilimtafuta Bwana; usiku niliinua mikono yangu, nayo haikuchoka. Moyo wangu ulikataa kufarijiwa.
In the day of my trouble I seek the Lord; with my hand uplifted, mine eye streameth in the night without ceasing; my soul refuseth to be comforted.
3 Ningali nikiugua nilielekeza mawazo yangu kwa Mungu. Nilimfikiria Mungu nilipokuwa dhaifu. (Selah)
When I think thereon, O God, I must moan; when I muse thereon, my spirit fainteth. (Selah)
4 Uliyafanya macho yangu yasisinzie; nilisumbuka sana kuongea.
Thou holdest fast the lids of mine eyes; I am troubled, and cannot speak.
5 Nilifikiri kuhusu siku za kale, kuhusu mambo yaliyopita muda mrefu.
I have pondered the days of old, the years of ancient times.
6 Wakati wa usiku niliukumbuka wimbo niliouimba mara moja. Nilifikiria kwa makini na kujaribu kuelewa kile kilichokuwa kimetokea.
In the night I will call to remembrance my song; I will commune with mine own heart; and my spirit maketh diligent search:
7 Je, Mungu atanikataa milele? Je, hatanionesha tena huruma?
'Will the Lord cast off for ever? and will He be favourable no more?
8 Je, uaminifu wa agano lake ulikuwa umetoweka milele? Je, ahadi yake imeshindwa milele?
Is His mercy clean gone for ever? Is His promise come to an end for evermore?
9 Je, Mungu amesahau kuwa mwenye neema? Je, hasira yake imeifunga huruma yake? (Selah)
Hath God forgotten to be gracious? Hath He in anger shut up his compassions?' (Selah)
10 Nilisema, “Hii ni huzuni yangu: mabadiliko ya mkono wa kuume wa Aliye Juu dhidi yetu.”
And I say: 'This is my weakness, that the right hand of the Most High could change.
11 Lakini nitayakumbuka matendo yako, Yahwe; nitafikiri kuhusu matendo yako makuu yaliyopita.
I will make mention of the deeds of the LORD; yea, I will remember Thy wonders of old.
12 Nitayatafakari matendo yako yote nami nitayaishi.
I will meditate also upon all Thy work, and muse on Thy doings.'
13 Njia yako, Mungu, ni takatifu; ni mungu gani wa kulinganishwa na Mungu wetu aliye mkuu?
O God, Thy way is in holiness; who is a great god like unto God?
14 Wewe ni Mungu utendaye maajabu; wewe umeonesha nguvu zako kati ya mataifa.
Thou art the God that doest wonders; Thou hast made known Thy strength among the peoples.
15 Uliwapa watu wako ushindi kwa uweza wako mkuu - ukoo wa Yakobo na Yusufu. (Selah)
Thou hast with Thine arm redeemed Thy people, the sons of Jacob and Joseph. (Selah)
16 Maji yalikuona wewe, Mungu; maji yalikuona wewe, nayo yakaogopa; vina vya maji vilitetemeka.
The waters saw Thee, O God; the waters saw Thee, they were in pain; the depths also trembled.
17 Mawingu yalitiririsha maji chini; anga zito lilitoa sauti; mishale yako ilipita kati.
The clouds flooded forth waters; the skies sent out a sound; Thine arrows also went abroad.
18 Sauti yako kama ya radi ilisikika katika upepo; radi iliwasha dunia; nchi iliogopa na kutetemeka.
The voice of Thy thunder was in the whirlwind; the lightnings lighted up the world; the earth trembled and shook.
19 Njia yako ilipita baharini na mapito yako katika maji mengi, lakini alama za miguu yako hazikuonekana.
Thy way was in the sea, and Thy path in the great waters, and Thy footsteps were not known.
20 Uliwaongoza watu wako kama kundi kwa mkono wa Musa na Haruni.
Thou didst lead Thy people like a flock, by the hand of Moses and Aaron.

< Zaburi 77 >