< Zaburi 76 >

1 Mungu amefanya mwenyewe kujulikana katika Yuda; jina lake ni kuu katika Israeli.
For the Chief Musician; on stringed instruments. A Psalm of Asaph, a Song. In Judah is God known: his name is great in Israel.
2 Hema yake iko salemu; makao yake yako yako Sayuni.
In Salem also is his tabernacle, and his dwelling place in Zion.
3 Huko ndiko alivunja mishale ya upinde, ngao, upanga, na silaha zingine za vita. (Selah)
There he brake the arrows of the bow; the shield, and the sword, and the battle. (Selah)
4 Wewe unang'aa sana na huufunua utukufu wako, ushukapo kutoka milimani, ambako uliwauwa mateka.
Glorious art thou [and] excellent, from the mountains of prey.
5 Wenye moyo shujaa walitekwa nyara; walilala mauti. Mashujaa wote walikuwa wanyonge.
The stouthearted are spoiled, they have slept their sleep; and none of the men of might have found their hands.
6 Kwa kukemea kwako, ewe Mungu wa Yakobo, wote gari na farasi walilala mauti.
At thy rebuke, O God of Jacob, both chariot and horse are cast into a dead sleep.
7 Wewe, ndiyo wewe, ni wa kuogopwa; ni nani awezaye kusimama mbele yako wakati ukiwa na hasira?
Thou, even thou, art to be feared: and who may stand in thy sight when once thou art angry?
8 Kutoka mbinguni wewe uliifanya hukumu yako isikike; nchi iliogopa na ikaa kimya
Thou didst cause sentence to be heard from heaven; the earth feared, and was still,
9 wakati wewe, Mungu, ulipoinuka kutekeleza hukumu na kuwaokoa wote wa nchi walio onewa. (Selah)
When God arose to judgment, to save all the meek of the earth. (Selah)
10 Hakika hukumu ya hasira yako dhidi ya binadamu itakuletea wewe sifa; wewe hujifunga mwenyewe hasira yako iliyo baki.
Surely the wrath of man shall praise thee: the residue of wrath shalt thou gird upon thee.
11 Wekeni nadhiri kwa Yahwe Mungu wenu na kuzihifadhi. Nao wote wamzungukao yeye mleteeni zawadi yeye ambaye ni wa kuogopwa.
Vow, and pay unto the LORD your God: let all that be round about him bring presents unto him that ought to be feared.
12 Yeye huzikata roho za wakuu; huogopwa na wafalme wa nchi.
He shall cut off the spirit of princes: he is terrible to the kings of the earth.

< Zaburi 76 >