< Zaburi 69 >

1 Uniokoe, Mungu; maana maji yameweka uhai wangu hatarini.
For the Chief Musician; set to Shoshannim. [A Psalm] of David. Save me, O God; for the waters are come in unto my soul.
2 Ninazama kwenye kina cha matope, pasipo na hahari pa kusimama; nimekuja kwenye kina kirefu cha maji, ambako mafuriko yananifunika.
I sink in deep mire, where there is no standing: I am come into deep waters, where the floods overflow me.
3 Nimechoka sana kwa kulia kwangu; koo langu ni kavu; macho yangu yanafifia wakati namngoja Mungu wangu.
I am weary with my crying; my throat is dried: mine eyes fail while I wait for my God.
4 Wale wanichukiao bila sababu wako zaidi ya nywele za kichwa changu; wale ambao wangeweza kuniua, wakiwa adui zangu kwa sababu zisizo sahihi, ni wengi mno; wanalazimisha nirudishe kile ambacho sijaiba.
They that hate me without a cause are more than the hairs of mine head: they that would cut me off, being mine enemies wrongfully, are mighty: then I restored that which I took not away.
5 Mungu, wewe unaujua ujinga wangu, na dhambi zangu hazifichiki kwako.
O God, thou knowest my foolishness; and my sins are not hid from thee.
6 Usiwaache wale wanao kungoja wewe waaibishwe kwa sababu yangu, Bwana Yahwe wa majeshi; usiwaache wale wanaokutafuta wewe wadharauliwe kwa sababu yangu, Mungu wa Israeli.
Let not them that wait on thee be ashamed through me, O Lord GOD of hosts: let not those that seek thee be brought to dishonour through me, O God of Israel.
7 Kwa ajili yako nimestahimili lawama; aibu imeufunika uso wangu.
Because for thy sake I have borne reproach; shame hath covered my face.
8 Nimekuwa mgeni kwa ndugu zangu, nisiye fahamika wala kuaminika kwa watoto wa mama yangu.
I am become a stranger unto my brethren, and an alien unto my mother’s children.
9 Kwa maana bidii ya nyumba yako imenila, na laumu zao wanao kulaumu wewe zimeniangukia mimi.
For the zeal of thine house hath eaten me up; and the reproaches of them that reproach thee are fallen upon me.
10 Wakati nilipolia na kutokula chakula, walinitukana.
When I wept, [and chastened] my soul with fasting, that was to my reproach.
11 Nilipoteneneza mavazi ya gunia, nikawa kituko kwao.
When I made sackcloth my clothing, I became a proverb unto them.
12 Wale wakaao katika lango la mji huniseng'enya; mimi ni wimbo wa walevi.
They that sit in the gate talk of me; and [I am] the song of the drunkards.
13 Lakini kwangu mimi, maombi yangu ni kwako, Yahwe, wakati ambao wewe utayapokea; unijibu katika uaminifu wa wokovu wako.
But as for me, my prayer is unto thee, O LORD, in an acceptable time: O God, in the multitude of thy mercy, answer me in the truth of thy salvation.
14 Unitoe matopeni, na usiniache nizame; uniondoe mbali na wale wanaonichukia na uniokoe katika kina cha maji.
Deliver me out of the mire, and let me not sink: let me be delivered from them that hate me, and out of the deep waters.
15 Usiache mafuliko ya maji yanielemee, wala kina kisinimeze. Usiache mdomo wa shimo unimeze.
Let not the waterflood overwhelm me, neither let the deep swallow me up; and let not the pit shut her mouth upon me.
16 Unijibu, Yahwe, maana uaminifu wa agano lako ni mwema; kwa maana rehema zako kwangu ni nyingi, unigeukie.
Answer me, O LORD; for thy lovingkindness is good: according to the multitude of thy tender mercies turn thou unto me.
17 Usiufiche uso wako mbali na mtumishi wako, maana niko katika dhiki; unijibu haraka.
And hide not thy face from thy servant; for I am in distress; answer me speedily.
18 Uje kwangu na unikomboe. Kwa sababu ya adui zangu, uwe fidia yangu.
Draw nigh unto my soul, and redeem it: ransom me because of mine enemies.
19 Wewe wajua kulaumiwa kwangu, kuaibishwa kwangu, na kudharauliwa kwangu; wapinzani wangu wote wako mbele yako.
Thou knowest my reproach, and my shame, and my dishonour: mine adversaries are all before thee.
20 Lawama imevunja moyo wangu; nimejawa na huzuni kubwa; nilitafuta mtu wa kunihurumia, lakini hakuwepo; nilitafuta wafariji, lakini sikupata.
Reproach hath broken my heart; and I am full of heaviness: and I looked for some to take pity, but there was none; and for comforters, but I found none.
21 Walinipa sumu kwa ajili ya chakula changu; katika kiu yangu walinipa siki ninywe.
They gave me also gall for my meat; and in my thirst they gave me vinegar to drink.
22 Meza yao mbele yao na iwe mtego; wafikiripo wako kwenye usalama, iwe kitanzi.
Let their table before them become a snare; and when they are in peace, [let it become] a trap.
23 Macho yao na yatiwe giza ili kwamba wasiweze kuona; uvifanye viuno vyao kutetemeka daima.
Let their eyes be darkened, that they see not; and make their loins continually to shake.
24 Wamwagie gadhabu yako, ukali wa hasira yako uwafikie wao.
Pour out thine indignation upon them, and let the fierceness of thine anger overtake them.
25 Sehemu yao na iwe ukiwa; mtu yeyote asiishi katika hema yao.
Let their habitation be desolate; let none dwell in their tents.
26 Kwa kuwa walimtesa yule uliyempa adhabu. Mara kwa mara walihesabu maumivu ya wale walioumizwa.
For they persecute him whom thou hast smitten; and they tell of the sorrow of those whom thou hast wounded,
27 Wakiwashtaki kuwa wamefanya uovu juu ya uovu; usiwaache waje kwenye ushindi wa haki yako.
Add iniquity unto their iniquity: and let them not come into thy righteousness.
28 Uwafute kwenye Kitabu cha Uzima na wasiandikwe pamoja na wenyehaki.
Let them be blotted out of the book of life, and not be written with the righteous.
29 Lakini mimi ni maskini na mwenye huzuni; uruhusu wokovu wako, Mungu, uniweke juu sana.
But I am poor and sorrowful: let thy salvation, O God, set me up on high.
30 Nitalisifu jina la Mungu kwa wimbo na nitamtukuza yeye kwa shukrani.
I will praise the name of God with a song, and will magnify him with thanksgiving.
31 Nitamsifu Yahwe zaidi kuliko ng'ombe au ndama aliye na mapembe na kwato.
And it shall please the LORD better than an ox, [or] a bullock that hath horns and hoofs.
32 Wanyenyekevu wameona na kufurahi; ninyi mnao matafuta Mungu, mioyo yenu itiwe nguvu.
The meek have seen it, and are glad: ye that seek after God, let your heart live.
33 Maana Yahwe husikia wenye uhitaji naye hawadharau wafungwa wake.
For the LORD heareth the needy, and despiseth not his prisoners.
34 Mbingu na nchi zimsifu yeye, bahari na vyote vitembeavyo majini.
Let heaven and earth praise him, the seas, and every thing that moveth therein.
35 Kwa maana Mungu ataiokoa Sayuni na ataujenga tena mji wa Yuda; watu wataishi huko na kupata umiliki wao.
For God will save Zion, and build the cities of Judah; and they shall abide there, and have it in possession.
36 Ukoo wa watumishi wake watairithi; nao walipendao jina lake wataishi humo.
The seed also of his servants shall inherit it; and they that love his name shall dwell therein.

< Zaburi 69 >