< Zaburi 75 >

1 Tunatoa shukrani kwako, Mungu; tunatoa shukrani, maana wewe unaufunua uwepo wako; watu huzungumza kuhusu kazi zako za ajabu.
For the Leader; Al-tashheth. A Psalm of Asaph, a Song. We give thanks unto Thee, O God, we give thanks, and Thy name is near; men tell of Thy wondrous works.
2 Kwa wakati maalum nitahukumu kwa haki.
'When I take the appointed time, I Myself will judge with equity.
3 Ingawa nchi na wenyeji wote watatikisika katika hofu, ninaifanyia nchi nguzo za kutosha. (Selah)
When the earth and all the inhabitants thereof are dissolved, I Myself establish the pillars of it.' (Selah)
4 Nilisema kwa wenye kiburi, “Msiwe wenye kiburi,” na kwa waovu, “Msiinue mapembe.
I say unto the arrogant: 'Deal not arrogantly'; and to the wicked: 'Lift not up the horn.'
5 Msiinue mapembe yenu kwenye marefu; wala msizungumze kwa shingo ya kiburi.”
Lift not up your horn on high; speak not insolence with a haughty neck.
6 Sio kutoka mashariki au magharibi, na wala sio kutoka jangwani ambako kuinuliwa kunakuja.
For neither from the east, nor from the west, nor yet from the wilderness, cometh lifting up.
7 Bali Mungu ni muhumkumu; humshusha huyu na kumuinua huyu.
For God is judge; He putteth down one, and lifteth up another.
8 Kwa kuwa Yahwe kashikilia mkononi mwake kikombe cha mvinyo wenye povu, ambao umechanganywa na vilolezo, naye huimimina. Hakika waovu wote wa duniani watakunywa mvinyo hadi tone la mwisho.
For in the hand of the LORD there is a cup, with foaming wine, full of mixture, and He poureth out of the same; surely the dregs thereof, all the wicked of the earth shall drain them, and drink them.
9 Bali mimi nitaendelea kusema yale ambayo umeyatenda; nami nitamwimbia sifa Mungu wa Yakobo.
But as for me, I will declare for ever, I will sing praises to the God of Jacob.
10 Yeye husema, “Nitayakata mapembe yote ya waovu, lakini mapembe ya wenye haki yatainuliwa.”
All the horns of the wicked also will I cut off; but the horns of the righteous shall be lifted up.

< Zaburi 75 >