< Zaburi 74 >

1 Mungu, kwa nini umetukataa milele? Kwa nini hasira yako inawaka dhidi ya kondoo wa malisho yako?
Pour instruire. D’Asaph. Pourquoi, ô Dieu, [nous] as-tu rejetés pour toujours, [et] ta colère fume-t-elle contre le troupeau de ta pâture?
2 Wafikilie watu wako, ambao uliwanunua siku nyingi zilizopita, kabila ambalo wewe umelikomboa liwe urithi wako, na Milima Sayuni, mahali uishipo.
Souviens-toi de ton assemblée, que tu as acquise autrefois, que tu as rachetée pour être la portion de ton héritage, – de la montagne de Sion, où tu as habité.
3 Uje utazame uharibifu kamili, uharibifu ambao umefanywa na adui mahali patakatifu.
Élève tes pas vers les ruines perpétuelles; l’ennemi a tout saccagé dans le lieu saint.
4 Washindani wako walivamia katikati ya mahali pako maalumu; walipandisha bendera zao za vita.
Tes adversaires rugissent au milieu des lieux assignés pour ton service; ils ont mis leurs signes pour signes.
5 Walipakatakata kwa shoka kama katika msitu mnene.
Un homme se faisait connaître quand il élevait la hache dans l’épaisseur de la forêt;
6 Walipaharibu na kuvunja sanaa zilizonakshiwa zote; walizivunja kwa shoka na nyundo.
Et maintenant, avec des cognées et des marteaux, ils brisent ses sculptures toutes ensemble.
7 Walipachoma patakatifu pako; walipanajisi mahari unapoishi, wakigongagonga kwenye ardhi.
Ils ont mis le feu à ton sanctuaire, ils ont profané par terre la demeure de ton nom;
8 Walisema mioyoni mwao, “Tutawaharibu wote.” Walichoma sehemu zako zote za kukutania katika nchi.
Ils ont dit en leur cœur: Détruisons-les tous ensemble. Ils ont brûlé tous les lieux assignés [pour le service] de Dieu dans le pays.
9 Sisi hatuoni tena ishara; hakuna tena nabii, na hakuna yeyote miongoni mwetu ajuaye haya yatadumu kwa muda gani.
Nous ne voyons plus nos signes; il n’y a plus de prophète, et il n’y a personne avec nous qui sache jusques à quand.
10 Mpaka lini, Mungu, adui atakurushia wewe matusi? Je, atalitukana jina lako milele?
Jusques à quand, ô Dieu! l’adversaire dira-t-il des outrages? L’ennemi méprisera-t-il ton nom à jamais?
11 Kwa nini umerudisha nyuma mkono wako, mkono wako wa kuume? Utoe mkono wako kwenye mavazi yako na uwaangamize.
Pourquoi détournes-tu ta main, et ta droite? [Tire-la] de ton sein: détruis!
12 Lakini Mungu amekuwa mfalme wangu tangu enzi, akileta wokovu tuniani.
Et Dieu est d’ancienneté mon roi, opérant des délivrances au milieu de la terre.
13 Wewe uliigawa bahari; ulishambulia vichwa vya majitu ya kutisha baharini majini.
Tu as fendu la mer par ta puissance, tu as brisé les têtes des monstres sur les eaux;
14 Wewe ulishambulia vichwa vya lewiathani; na kumfanya awe chakula cha viumbe hai jangwani.
Tu as écrasé les têtes du léviathan, tu l’as donné pour pâture au peuple, – aux bêtes du désert.
15 Ulizifungulia chemchem na vijito; uliikausha mito itiririkayo.
Tu as fait sortir la source et le torrent; tu as séché les grosses rivières.
16 Mchana ni wako, na usiku ni wako pia; uliweka jua na mwezi mahari pake.
À toi est le jour, à toi aussi la nuit; toi tu as établi la lune et le soleil.
17 Umeiweka mipaka ya nchi; umeumba majira ya joto na majira ya baridi.
Tu as posé toutes les bornes de la terre; l’été et l’hiver, c’est toi qui les as formés.
18 Kumbula vile adui alivyo vurumisha matusi kwako, Yahwe, na kwamba watu wapumbavu wamelitukana jina lako.
Souviens-toi de ceci, que l’ennemi a outragé l’Éternel! et qu’un peuple insensé a méprisé ton nom.
19 Usimtoe njiwa afe kwa mnyama wa porini. Usiusahau milele uhai wa watu wako walio onewa.
Ne livre pas à la bête sauvage l’âme de ta tourterelle; n’oublie pas à jamais la troupe de tes affligés.
20 Kumbuka agano lako, maana majimbo ya giza ya nchi yamejaa maeneo ya vurugu.
Regarde à l’alliance! Car les lieux ténébreux de la terre sont pleins d’habitations de violence.
21 Usiwaache walioonewa warudishwe kwa aibu; uwaache maskini na walioonewa walisifu jina lako.
Que l’opprimé ne s’en retourne pas confus; que l’affligé et le pauvre louent ton nom.
22 Inuka Mungu, itetee heshima yako; kumbuka wajinga wanavyokutukana machana kutwa.
Lève-toi, ô Dieu! plaide ta cause, souviens-toi des outrages que te fait tous les jours l’insensé.
23 Usisahau sauti ya adui zako au kelele za wale wanaoendelea kukuchafua.
N’oublie pas la voix de tes adversaires: le tumulte de ceux qui s’élèvent contre toi monte continuellement.

< Zaburi 74 >