< Zaburi 74 >

1 Mungu, kwa nini umetukataa milele? Kwa nini hasira yako inawaka dhidi ya kondoo wa malisho yako?
An Instruction of Asaph. Why, O God, hast Thou cast off for ever? Thine anger smoketh against the flock of Thy pasture.
2 Wafikilie watu wako, ambao uliwanunua siku nyingi zilizopita, kabila ambalo wewe umelikomboa liwe urithi wako, na Milima Sayuni, mahali uishipo.
Remember Thy company. Thou didst purchase of old, Thou didst redeem the rod of Thy inheritance, This mount Zion — Thou didst dwell in it.
3 Uje utazame uharibifu kamili, uharibifu ambao umefanywa na adui mahali patakatifu.
Lift up Thy steps to the perpetual desolations, Everything the enemy did wickedly in the sanctuary.
4 Washindani wako walivamia katikati ya mahali pako maalumu; walipandisha bendera zao za vita.
Roared have thine adversaries, In the midst of Thy meeting-places, They have set their ensigns as ensigns.
5 Walipakatakata kwa shoka kama katika msitu mnene.
He is known as one bringing in on high Against a thicket of wood — axes.
6 Walipaharibu na kuvunja sanaa zilizonakshiwa zote; walizivunja kwa shoka na nyundo.
And now, its carvings together With axe and hatchet they break down,
7 Walipachoma patakatifu pako; walipanajisi mahari unapoishi, wakigongagonga kwenye ardhi.
They have sent into fire Thy sanctuary, to the earth they polluted the tabernacle of Thy name,
8 Walisema mioyoni mwao, “Tutawaharibu wote.” Walichoma sehemu zako zote za kukutania katika nchi.
They said in their hearts, 'Let us oppress them together,' They did burn all the meeting-places of God in the land.
9 Sisi hatuoni tena ishara; hakuna tena nabii, na hakuna yeyote miongoni mwetu ajuaye haya yatadumu kwa muda gani.
Our ensigns we have not seen, There is no more a prophet, Nor with us is one knowing how long.
10 Mpaka lini, Mungu, adui atakurushia wewe matusi? Je, atalitukana jina lako milele?
Till when, O God, doth an adversary reproach? Doth an enemy despise thy name for ever?
11 Kwa nini umerudisha nyuma mkono wako, mkono wako wa kuume? Utoe mkono wako kwenye mavazi yako na uwaangamize.
Why dost Thou turn back Thy hand, Even Thy right hand? From the midst of Thy bosom remove [it].
12 Lakini Mungu amekuwa mfalme wangu tangu enzi, akileta wokovu tuniani.
And God [is] my king of old, Working salvation in the midst of the earth.
13 Wewe uliigawa bahari; ulishambulia vichwa vya majitu ya kutisha baharini majini.
Thou hast broken by Thy strength a sea -[monster], Thou hast shivered Heads of dragons by the waters,
14 Wewe ulishambulia vichwa vya lewiathani; na kumfanya awe chakula cha viumbe hai jangwani.
Thou hast broken the heads of leviathan, Thou makest him food, For the people of the dry places.
15 Ulizifungulia chemchem na vijito; uliikausha mito itiririkayo.
Thou hast cleaved a fountain and a stream, Thou hast dried up perennial flowings.
16 Mchana ni wako, na usiku ni wako pia; uliweka jua na mwezi mahari pake.
Thine [is] the day, also Thine [is] the night, Thou hast prepared a light giver — the sun.
17 Umeiweka mipaka ya nchi; umeumba majira ya joto na majira ya baridi.
Thou hast set up all the borders of earth, Summer and winter Thou hast formed them.
18 Kumbula vile adui alivyo vurumisha matusi kwako, Yahwe, na kwamba watu wapumbavu wamelitukana jina lako.
Remember this — an enemy reproached Jehovah, And a foolish people have despised Thy name.
19 Usimtoe njiwa afe kwa mnyama wa porini. Usiusahau milele uhai wa watu wako walio onewa.
Give not up to a company, The soul of Thy turtle-dove, The company of Thy poor ones forget not for ever.
20 Kumbuka agano lako, maana majimbo ya giza ya nchi yamejaa maeneo ya vurugu.
Look attentively to the covenant, For the dark places of earth, Have been full of habitations of violence.
21 Usiwaache walioonewa warudishwe kwa aibu; uwaache maskini na walioonewa walisifu jina lako.
Let not the oppressed turn back ashamed, Let the poor and needy praise Thy name,
22 Inuka Mungu, itetee heshima yako; kumbuka wajinga wanavyokutukana machana kutwa.
Arise, O God, plead Thy plea, Remember Thy reproach from a fool all the day.
23 Usisahau sauti ya adui zako au kelele za wale wanaoendelea kukuchafua.
Forget not the voice of Thine adversaries, The noise of Thy withstanders is going up continually!

< Zaburi 74 >