< Zaburi 74 >

1 Mungu, kwa nini umetukataa milele? Kwa nini hasira yako inawaka dhidi ya kondoo wa malisho yako?
[A contemplation by Asaph.] God, why have you rejected us forever? Why does your anger smolder against the sheep of your pasture?
2 Wafikilie watu wako, ambao uliwanunua siku nyingi zilizopita, kabila ambalo wewe umelikomboa liwe urithi wako, na Milima Sayuni, mahali uishipo.
Remember your congregation, which you purchased of old, which you have redeemed to be the tribe of your inheritance; Mount Zion, in which you have lived.
3 Uje utazame uharibifu kamili, uharibifu ambao umefanywa na adui mahali patakatifu.
Lift up your feet to the perpetual ruins, all the evil that the enemy has done in the sanctuary.
4 Washindani wako walivamia katikati ya mahali pako maalumu; walipandisha bendera zao za vita.
Your adversaries have roared in the midst of your assembly. They have set up their standards as signs.
5 Walipakatakata kwa shoka kama katika msitu mnene.
They behaved like men wielding axes, cutting through a thicket of trees.
6 Walipaharibu na kuvunja sanaa zilizonakshiwa zote; walizivunja kwa shoka na nyundo.
Now they break all its carved work down with hatchet and hammers.
7 Walipachoma patakatifu pako; walipanajisi mahari unapoishi, wakigongagonga kwenye ardhi.
They have burned your sanctuary to the ground. They have profaned the dwelling place of your Name.
8 Walisema mioyoni mwao, “Tutawaharibu wote.” Walichoma sehemu zako zote za kukutania katika nchi.
They said in their heart, "We will crush them completely." They have burned up all the places in the land where God was worshiped.
9 Sisi hatuoni tena ishara; hakuna tena nabii, na hakuna yeyote miongoni mwetu ajuaye haya yatadumu kwa muda gani.
We see no miraculous signs. There is no longer any prophet, neither is there among us anyone who knows how long.
10 Mpaka lini, Mungu, adui atakurushia wewe matusi? Je, atalitukana jina lako milele?
How long, God, shall the enemy mock? Shall the enemy blaspheme your name forever?
11 Kwa nini umerudisha nyuma mkono wako, mkono wako wa kuume? Utoe mkono wako kwenye mavazi yako na uwaangamize.
Why do you draw back your hand, even your right hand? Take it out of your pocket and consume them.
12 Lakini Mungu amekuwa mfalme wangu tangu enzi, akileta wokovu tuniani.
Yet God is my King from long ago, working salvation in the midst of the earth.
13 Wewe uliigawa bahari; ulishambulia vichwa vya majitu ya kutisha baharini majini.
You divided the sea by your strength. You broke the heads of the sea monsters in the waters.
14 Wewe ulishambulia vichwa vya lewiathani; na kumfanya awe chakula cha viumbe hai jangwani.
You broke the heads of Leviathan in pieces. You gave him as food to people and desert creatures.
15 Ulizifungulia chemchem na vijito; uliikausha mito itiririkayo.
You opened up spring and stream. You dried up mighty rivers.
16 Mchana ni wako, na usiku ni wako pia; uliweka jua na mwezi mahari pake.
The day is yours, the night is also yours. You have prepared the light and the sun.
17 Umeiweka mipaka ya nchi; umeumba majira ya joto na majira ya baridi.
You have set all the boundaries of the earth. You have made summer and winter.
18 Kumbula vile adui alivyo vurumisha matusi kwako, Yahwe, na kwamba watu wapumbavu wamelitukana jina lako.
Remember this, that the enemy has mocked you, LORD. Foolish people have blasphemed your name.
19 Usimtoe njiwa afe kwa mnyama wa porini. Usiusahau milele uhai wa watu wako walio onewa.
Do not deliver the soul of your dove to wild beasts. Do not forget the life of your poor forever.
20 Kumbuka agano lako, maana majimbo ya giza ya nchi yamejaa maeneo ya vurugu.
Honor your covenant, for haunts of violence fill the dark places of the earth.
21 Usiwaache walioonewa warudishwe kwa aibu; uwaache maskini na walioonewa walisifu jina lako.
Do not let the oppressed return ashamed. Let the poor and needy praise your name.
22 Inuka Mungu, itetee heshima yako; kumbuka wajinga wanavyokutukana machana kutwa.
Arise, God. Plead your own cause. Remember how the foolish man mocks you all day.
23 Usisahau sauti ya adui zako au kelele za wale wanaoendelea kukuchafua.
Do not forget the voice of your adversaries. The tumult of those who rise up against you ascends continually.

< Zaburi 74 >