< Zaburi 74 >

1 Mungu, kwa nini umetukataa milele? Kwa nini hasira yako inawaka dhidi ya kondoo wa malisho yako?
阿撒夫的訓誨詩。 天主,您為何常久棄捨不管,對您牧場的羊群怒火炎炎?
2 Wafikilie watu wako, ambao uliwanunua siku nyingi zilizopita, kabila ambalo wewe umelikomboa liwe urithi wako, na Milima Sayuni, mahali uishipo.
求您懷念您自古所佔有的會伴,您所贖回給您作產業的族團,及您在那裏設置寶座的熙雍山,
3 Uje utazame uharibifu kamili, uharibifu ambao umefanywa na adui mahali patakatifu.
求您舉步踏向久存的荒野:敵人在聖所中摧毀了一切。
4 Washindani wako walivamia katikati ya mahali pako maalumu; walipandisha bendera zao za vita.
您的仇人在您的會場上咆哮狂謾,豎立起自己的旗幟作為凱旋紀念。
5 Walipakatakata kwa shoka kama katika msitu mnene.
他們相似高舉斧子的樵夫,在森林中砍伐堅硬的樹木。
6 Walipaharibu na kuvunja sanaa zilizonakshiwa zote; walizivunja kwa shoka na nyundo.
他們竟用斧頭鐵鎚,搗毀了聖殿的門扉;
7 Walipachoma patakatifu pako; walipanajisi mahari unapoishi, wakigongagonga kwenye ardhi.
他們又縱火焚燒了您的聖殿,把您聖名的居所褻瀆於地面。
8 Walisema mioyoni mwao, “Tutawaharibu wote.” Walichoma sehemu zako zote za kukutania katika nchi.
心裏說:我們把它們全部摧毀,燒盡天主在地上所有的殿宇。
9 Sisi hatuoni tena ishara; hakuna tena nabii, na hakuna yeyote miongoni mwetu ajuaye haya yatadumu kwa muda gani.
我們的標幟,已再不見,一個先知也不復出現,我們都不知幾時纔完。
10 Mpaka lini, Mungu, adui atakurushia wewe matusi? Je, atalitukana jina lako milele?
天主,仇人欺凌辱罵要到何時﹖敵人豈能永遠褻瀆您的名字?
11 Kwa nini umerudisha nyuma mkono wako, mkono wako wa kuume? Utoe mkono wako kwenye mavazi yako na uwaangamize.
為何您把您的手收回,將您的右手插入懷裏?
12 Lakini Mungu amekuwa mfalme wangu tangu enzi, akileta wokovu tuniani.
天主,從古以來是我的君主,是他在人世間實行了救助。
13 Wewe uliigawa bahari; ulishambulia vichwa vya majitu ya kutisha baharini majini.
您以您的權能分開了大海,在水中擊破了毒龍的頭蓋。
14 Wewe ulishambulia vichwa vya lewiathani; na kumfanya awe chakula cha viumbe hai jangwani.
打碎了里外雅堂的頭顱,且將牠作為海怪的食物。
15 Ulizifungulia chemchem na vijito; uliikausha mito itiririkayo.
您引源泉溪水流滾涓涓,卻使洶湧江河涸竭枯乾,
16 Mchana ni wako, na usiku ni wako pia; uliweka jua na mwezi mahari pake.
白日屬於您,黑夜也屬於您,月亮和太陽都是由您佈置。
17 Umeiweka mipaka ya nchi; umeumba majira ya joto na majira ya baridi.
您劃出了大地的界限,您制定了冬夏的時間。
18 Kumbula vile adui alivyo vurumisha matusi kwako, Yahwe, na kwamba watu wapumbavu wamelitukana jina lako.
上主求您切記:仇人褻瀆了您,無知的百姓侮辱了您的名字。
19 Usimtoe njiwa afe kwa mnyama wa porini. Usiusahau milele uhai wa watu wako walio onewa.
求您不要將您斑鳩的性命交給野鷹,永遠也不要忘記您的窮苦人的性命。
20 Kumbuka agano lako, maana majimbo ya giza ya nchi yamejaa maeneo ya vurugu.
求您回顧您所立的誓盟,因各地暗處充滿了強橫。
21 Usiwaache walioonewa warudishwe kwa aibu; uwaache maskini na walioonewa walisifu jina lako.
願受壓迫的人不要含羞回程,願貧苦窮乏的人歌頌您的名。
22 Inuka Mungu, itetee heshima yako; kumbuka wajinga wanavyokutukana machana kutwa.
天主,求您速來處理您的案件,切記糊塗人天天對您的侮慢。
23 Usisahau sauti ya adui zako au kelele za wale wanaoendelea kukuchafua.
千萬不要忘了您敵人的喧囂,和反抗您的人們不斷的狂叫。

< Zaburi 74 >