< Zaburi 64 >

1 Sikia sauti yangu, Mungu, usikilize malalamiko yangu; unilinde dhidi ya hofu ya adui zangu.
For the Leader. A Psalm of David. Hear my voice, O God, in my complaint; preserve my life from the terror of the enemy.
2 Unifiche dhidi ya mipango ya siri ya wafanyao maovu, unifiche dhidi ya watendao vurugu ya udhalimu.
Hide me from the council of evil-doers; from the tumult of the workers of iniquity;
3 Wao wamenoa ndimi zao kama panga; wamelenga mishale yao, maneno machungu,
Who have whet their tongue like a sword, and have aimed their arrow, a poisoned word;
4 ili kwamba waweze kupiga kutoka mahali pa siri kwenda kwa mtu asiye na hatia; wampige yeye kwa ghafla nao wasihofu lolote.
That they may shoot in secret places at the blameless; suddenly do they shoot at him, and fear not.
5 Wao wanahamasishana wenyewe katika kupanga uovu; wanashauriana pamoja wao binafsi ili kuweka mitego; nao husema, “Ni nani atakayetuona?”
They encourage one another in an evil matter; they converse of laying snares secretly; they ask, who would see them.
6 Wanabuni mipango ya dhambi; “Tumemaliza,” wanasema, “ni mpango makini.” Mawazo ya ndani na mioyo ya watu ni ya kina.
They search out iniquities, they have accomplished a diligent search; even in the inward thought of every one, and the deep heart.
7 Lakini Mungu atawapiga wao; ghafla watajeruhiwa kwa mishale yake.
But God doth shoot at them with an arrow suddenly; thence are their wounds.
8 Watafanywa kuwa mashakani, kwa kuwa ndimi zao wenyewe ziko kinyume nao; wote wawaonao watatikisa vichwa vyao.
So they make their own tongue a stumbling unto themselves; all that see them shake the head.
9 Watu wote wataogopa na kutangaza matendo ya Mungu. Kwa hekima watafikiria kuhusu kile yeye ametenda.
And all men fear; and they declare the work of God, and understand His doing.
10 Wenye haki watakuwa na furaha kuhusu Yahwe nao watakimbilia kwake; wote wenye haki moyoni watajivuna katika yeye.
The righteous shall be glad in the LORD, and shall take refuge in Him; and all the upright in heart shall glory.

< Zaburi 64 >