< Zaburi 62 >

1 Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; wokovu wangu watoka kwake.
For the Leader; for Jeduthun. A Psalm of David. Only for God doth my soul wait in stillness; from Him cometh my salvation.
2 Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa kamwe.
He only is my rock and my salvation, my high tower, I shall not be greatly moved.
3 Mpaka lini, ninyi nyote, mtamshambulia mtu, ili kwamba mumpindue yeye kama ukuta ulio inama au kama fensi isiyo imara?
How long will ye set upon a man, that ye may slay him, all of you, as a leaning wall, a tottering fence?
4 Wanashauliana naye ili tu kumshusha chini kutoka kwenye nafasi yake heshimiwa; wao wanapenda kuongea uongo; wanambariki yeye kwa midomo yao, lakini mioyoni mwao wana mlaani yeye. (Selah)
They only devise to thrust him down from his height, delighting in lies; they bless with their mouth, but they curse inwardly. (Selah)
5 Katika ukimya ninamsubiri Mungu pekee; kwa maana matumaini yangu yako kwake.
Only for God wait thou in stillness, my soul; for from Him cometh my hope.
6 Yeye pekee ni mwamba wangu na wokovu wangu; yeye ni mnara wangu mrefu; sitasogezwa.
He only is my rock and my salvation, my high tower, I shall not be moved.
7 Na Mungu ni wokovu wangu na utukufu wangu; mwamba wa nguvu yangu na kimbilio langu salama liko katika Mungu.
Upon God resteth my salvation and my glory; the rock of my strength, and my refuge, is in God.
8 Mwaminini Mungu wakati wote, ninyi watu; mimina moyo wako mbele zake; Mungu ni kimbilio salama kwa ajili yetu. (Selah)
Trust in Him at all times, ye people; pour out your heart before Him; God is a refuge for us. (Selah)
9 Hakika watu wenye msimamo mdogo ni ubatili, na watu wenye msimamo mkubwa ni waongo; wao watakuwa wepesi kwenye mzani; uzito wao pamoja ni wepesi kuliko kitu chochote.
Men of low degree are vanity, and men of high degree are a lie; if they be laid in the balances, they are together lighter than vanity.
10 Usiamini katika ukandamizaji au wizi; usitumainie utajiri, maana hawatazaa matunda; usiuweke moyo wako kwenye hivyo.
Trust not in oppression, and put not vain hope in robbery; if riches increase, set not your heart thereon.
11 Mungu ameongea mara moja, mara mbili nimesikia hili: nguvu ni za Mungu.
God hath spoken once, twice have I heard this: that strength belongeth unto God;
12 Pia kwako, Bwana, ni uaminifu wa agano, maana humlipa kila mtu kwa kile alichokifanya.
Also unto Thee, O Lord, belongeth mercy; for Thou renderest to every man according to his work.

< Zaburi 62 >