< Zaburi 60 >

1 Mungu, wewe umetutupa; umeuvunja ulinzi wetu; wewe umekuwa hasirani; utuwezeshe tena.
For the Chief Musician; set to Shushan Eduth: Michtam of David, to teach: when he strove with Aram-naharaim and with Aram-zobah, and Joab returned, and smote of Edom in the Valley of Salt twelve thousand. O God, thou hast cast us off, thou hast broken us down; thou hast been angry; O restore us again.
2 Wewe umeifanya nchi kutetemeka; umeipasua pasua; uiponye nyufa zake, maana zinatikisika.
Thou hast made the land to tremble; thou hast rent it: heal the breaches thereof; for it shaketh.
3 Wewe umewafanya watu wako kuona mambo magumu; umetufanya tunywe mvinyo wenye kutufanya kupepesuka.
Thou hast shewed thy people hard things: thou hast made us to drink the wine of staggering.
4 Kwa wale wanao kuheshimu wewe, wewe umeweka bandera ionekane dhidi ya wale wabebao upinde. (Selah)
Thou hast given a banner to them that fear thee, that it may be displayed because of the truth. (Selah)
5 Ili kwamba wale uwapendao waweze kuokolewa, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
That thy beloved may be delivered, save with thy right hand, and answer us.
6 Mungu ameongea katika utakatifu wake, “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na kuligawa bonde la Sukothi.
God hath spoken in his holiness; I will exult: I will divide Shechem, and mete out the valley of Succoth.
7 Gileadi ni yangu, na Manase ni yangu na Ephraimu pia ni kofia yangu ya chuma; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
Gilead is mine, and Manasseh is mine; Ephraim also is the defence of mine head; Judah is my sceptre.
8 Moabu ni bakuli langu la kunawia; juu ya Edomu nitatupa kiatu changu; nitapiga kelele za ushindi kwa sababu ya Filisti.”
Moab is my washpot; upon Edom will I cast my shoe: Philistia, shout thou because of me.
9 Ni nani atakaye nileta kwenye mji imara? Ni nani ataniongoza kwenda Edomu?
Who will bring me into the strong city? who hath led me unto Edom?
10 Lakini wewe, Mungu, je, haukutukataa? Wewe hauendi vitani pamoja na jeshi letu.
Hast not thou, O God, cast us off? and thou goest not forth, O God, with our hosts.
11 Utusaidie dhidi ya adui yetu, maana msaada wa mwanadamu ni bure.
Give us help against the adversary: for vain is the help of man.
12 Kwa msaada wa Mungu tutashinda; yeye atawakanyaga chini adui zetu.
Through God we shall do valiantly: for he it is that shall tread down our adversaries.

< Zaburi 60 >