< Zaburi 60 >

1 Mungu, wewe umetutupa; umeuvunja ulinzi wetu; wewe umekuwa hasirani; utuwezeshe tena.
God, you have rejected us. You have broken us down. You have been angry. Restore us, again.
2 Wewe umeifanya nchi kutetemeka; umeipasua pasua; uiponye nyufa zake, maana zinatikisika.
You have made the land tremble. You have torn it. Mend its fractures, for it quakes.
3 Wewe umewafanya watu wako kuona mambo magumu; umetufanya tunywe mvinyo wenye kutufanya kupepesuka.
You have shown your people hard things. You have made us drink the wine that makes us stagger.
4 Kwa wale wanao kuheshimu wewe, wewe umeweka bandera ionekane dhidi ya wale wabebao upinde. (Selah)
You have given a banner to those who fear you, that it may be displayed because of the truth. (Selah) ·contemplation with musical interlude·.
5 Ili kwamba wale uwapendao waweze kuokolewa, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
So that your yadid ·beloved· may be delivered, save with your right hand, and answer us.
6 Mungu ameongea katika utakatifu wake, “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na kuligawa bonde la Sukothi.
God has spoken from his sanctuary: “I will triumph. I will divide Shechem, and measure out the valley of Sukkot.
7 Gileadi ni yangu, na Manase ni yangu na Ephraimu pia ni kofia yangu ya chuma; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
Gilead is mine, and Manasseh [Causing to forget] is mine. Ephraim [Fruit] also is the defense of my head. Judah [Praised] is my scepter.
8 Moabu ni bakuli langu la kunawia; juu ya Edomu nitatupa kiatu changu; nitapiga kelele za ushindi kwa sababu ya Filisti.”
Moab [From father] is my wash basin. I will throw my shoe on Edom [Red]. I shout in triumph over Philistia.”
9 Ni nani atakaye nileta kwenye mji imara? Ni nani ataniongoza kwenda Edomu?
Who will bring me into the strong city? Who has led me to Edom [Red]?
10 Lakini wewe, Mungu, je, haukutukataa? Wewe hauendi vitani pamoja na jeshi letu.
Haven’t you, God, rejected us? You don’t go out with our armies, God.
11 Utusaidie dhidi ya adui yetu, maana msaada wa mwanadamu ni bure.
Give us help against the adversary, for the help of man is vain.
12 Kwa msaada wa Mungu tutashinda; yeye atawakanyaga chini adui zetu.
Through God we shall do valiantly, for it is he who will tread down our adversaries.

< Zaburi 60 >