< Zaburi 57 >

1 Unihurumie, Mungu, unihurumie mimi, kwa maana ninakukimbilia wewe mpaka matatizo haya yaishe. Ninakaa chini ya mbawa za zako kwa ajili ya ulinzi mpaka huu uharibifu utakapoisha.
Be merciful to me, God, show favor to me, for my soul takes refuge in you. Yes, in the shadow of your wings, I will take refuge, until disaster has passed.
2 Nitakulilia Mungu uliye hai, kwa Mungu, afanyaye mambo yote kwa ajili yangu.
I cry out to El 'Elyon [God Most High], to God who accomplishes my requests for me.
3 Yeye atatuma msaada kutoka mbinguni na kuniokoa, ana hasira na wale wanaonishambulia. (Selah) Mungu atanitumia upendo wake mwema na uaminifu wake.
He will send from heaven, and save me, he rebukes the one who is pursuing me. (Selah) ·contemplation with musical interlude·. God will send out his cheshed ·loving-kindness· and his truth.
4 Uhai wangu uko katikati ya simba; niko katikati ya wale walio tayari kunila. Niko katikati ya watu ambao meno yao ni mikuki na mishale, na ambao ndimi zao ni kali kama upanga.
My soul is among lions. I lie among those who are set on fire, even the sons of men, whose teeth are spears and arrows, and their tongue a sharp sword.
5 Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu, utukufu wako uwe juu ya nchi yote.
Be exalted, God, above the heavens! Let your kavod ·weighty glory· be above all the earth!
6 Wao walisambaza nje wavu kwa ajili ya miguu yangu; nilikuwa na shida sana. Walichimba shimo mbele yangu. Wao wenyewe wameangukia katikati ya shimo! (Selah)
They have prepared a net for my steps. My soul is bowed down. They dig a pit before me. They fall into the middle of it themselves. (Selah) ·contemplation with musical interlude·.
7 Moyo wangu umeponywa, Mungu, moyo wangu umeponywa, nitaimba, ndiyo, nitaimba sifa.
My heart is steadfast, God, my heart is steadfast. I will sing, yes, I will sing zahmar ·musical praise·.
8 Inuka, moyo wa thamani; inuka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
Wake up, my glory! Wake up, lute and harp! I will wake up the dawn.
9 Nitakushukuru wewe, Bwana, kati ya watu; Kati ya mataifa nitakuimbia sifa.
I will yadah ·extend hands in thankful praise· to you, Lord, among the peoples. I will sing zahmar ·musical praise· to you among the nations.
10 Maana upendo wako usiokwisha, huzifikia mbingu; na uaminifu wako mawinguni.
For your great cheshed ·loving-kindness· reaches to the heavens, and your truth to the skies.
11 Uinuliwe, Mungu, juu ya mbingu; na utukufu wako uinuliwe juu ya nchi yote.
Be exalted, God, above the heavens. Let your kavod ·weighty glory· be over all the earth.

< Zaburi 57 >