< Zaburi 56 >

1 Uwe na huruma nami, Mungu, kwa maana watu wananishambulia! Muda wote wale wanao pigana nami hunikaribia zaidi ili wanishambulie.
Be merciful to me, God, for man wants to swallow me up. All day long, he attacks and oppresses me.
2 Adui zangu hunikanyaga muda wote; maana ni wengi ambao kwa kiburi hupigana dhidi yangu.
My enemies want to swallow me up all day long, for they are many who fight proudly against me.
3 Wakati nina woga, nitaweka imani yangu katika wewe.
When I am afraid, I will put my trust in you.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu - nimeweka imani yangu katika Mungu; sitaogopa; mtu wa kawaida atanifanya nini?
In God, I praise his word. In God, I put my trust. I will not be afraid. What can flesh do to me?
5 Muda wote wanayageuza maneno yangu; mawazo yao yote yako kinyume na mimi kwa ajili ya uovu.
All day long they twist my words. All their thoughts are against me for evil.
6 Wanajikusanya kwa pamoja, wanajificha wenyewe, na kuzifuatilia hatua zangu, wakisubiri kuniua.
They conspire and lurk, watching my steps, they are eager to take my life.
7 Usiwaache waikimbie adhabu yako kwa ajili ya uovu wao. Uwaangushe watu chini katika hasira yako, Mungu.
Shall they escape by iniquity? In anger cast down the peoples, God.
8 Wewe unahesabu kutangatanga kwangu na kuweka machozi yangu kwenye chupa yako; je, hayako kitabuni mwako?
You count my wanderings. You put my tears into your bottle. Are not they in your book?
9 Ndipo maadui zangu watakimbia katika siku ile nikuitapo wewe; hili najua, kwamba Mungu yupo kwa ajili yangu.
Then my enemies shall turn back in the day that I call. I know this, that God is for me.
10 Katika Mungu ambaye neno lake ninalisifu, katika Yahwe ambaye neno lake ninalisifu,
In God, I will praise his word. In Adonai, I will praise his word.
11 katika Mungu ninaamini, sitaogopa. Yeyote atanifanya nini?
I have put my trust in God. I will not be afraid. What can man do to me?
12 Wajibu wa kutimiza viapo vyangu kwako uko juu yangu, Mungu; nitatoa sadaka ya shukurani.
Your vows are on me, God. I will give thank offerings to you.
13 Kwa kuwa umeokoa uhai wangu na mauti; umezuia miguu yangu isianguke, ili kwamba niweze kutembea mbele ya Mungu katika nuru ya uhai.
For you have delivered my soul from death, and prevented my feet from falling, that I may walk before God in the light of the living.

< Zaburi 56 >