< Zaburi 56 >

1 Uwe na huruma nami, Mungu, kwa maana watu wananishambulia! Muda wote wale wanao pigana nami hunikaribia zaidi ili wanishambulie.
For the Leader; upon Jonath-elem-rehokim. A Psalm of David; Michtam; when the Philistines took him in Gath. Be gracious unto me, O God, for man would swallow me up; all the day he fighting oppresseth me.
2 Adui zangu hunikanyaga muda wote; maana ni wengi ambao kwa kiburi hupigana dhidi yangu.
They that lie in wait for me would swallow me up all the day; for they are many that fight against me, O Most High,
3 Wakati nina woga, nitaweka imani yangu katika wewe.
In the day that I am afraid, I will put my trust in Thee.
4 Katika Mungu, ambaye neno lake ninalisifu - nimeweka imani yangu katika Mungu; sitaogopa; mtu wa kawaida atanifanya nini?
In God — I will praise His word — in God do I trust, I will not be afraid; what can flesh do unto me?
5 Muda wote wanayageuza maneno yangu; mawazo yao yote yako kinyume na mimi kwa ajili ya uovu.
All the day they trouble mine affairs; all their thoughts are against me for evil.
6 Wanajikusanya kwa pamoja, wanajificha wenyewe, na kuzifuatilia hatua zangu, wakisubiri kuniua.
They gather themselves together, they hide themselves, they mark my steps; according as they have waited for my soul.
7 Usiwaache waikimbie adhabu yako kwa ajili ya uovu wao. Uwaangushe watu chini katika hasira yako, Mungu.
Because of iniquity cast them out; in anger bring down the peoples, O God.
8 Wewe unahesabu kutangatanga kwangu na kuweka machozi yangu kwenye chupa yako; je, hayako kitabuni mwako?
Thou has counted my wanderings; put Thou my tears into Thy bottle; are they not in Thy book?
9 Ndipo maadui zangu watakimbia katika siku ile nikuitapo wewe; hili najua, kwamba Mungu yupo kwa ajili yangu.
Then shall mine enemies turn back in the day that I call; this I know, that God is for me.
10 Katika Mungu ambaye neno lake ninalisifu, katika Yahwe ambaye neno lake ninalisifu,
In God — I will praise His word — in the LORD — I will praise His word —
11 katika Mungu ninaamini, sitaogopa. Yeyote atanifanya nini?
In God do I trust, I will not be afraid; what can man do unto me?
12 Wajibu wa kutimiza viapo vyangu kwako uko juu yangu, Mungu; nitatoa sadaka ya shukurani.
Thy vows are upon me, O God; I will render thank-offerings unto Thee.
13 Kwa kuwa umeokoa uhai wangu na mauti; umezuia miguu yangu isianguke, ili kwamba niweze kutembea mbele ya Mungu katika nuru ya uhai.
For thou hast delivered my soul from death; hast Thou not delivered my feet from stumbling? that I may walk before God in the light of the living.

< Zaburi 56 >