< Zaburi 52 >

1 Kwa nini wewe unajivunia kufanya uovu, wewe mtu mwenye nguvu? Uaminifu wa agano la Mungu huja kila siku.
For the Leader. Maschil of David; when Doeg the Edomite came and told Saul, and said unto him: 'David is come to the house of Ahimelech.' Why boastest thou thyself of evil, O mighty man? The mercy of God endureth continually.
2 Ulimi wako hupanga uharibifu kama wembe mkali, na kufanya udanganyifu.
Thy tongue deviseth destruction; like a sharp razor, working deceitfully.
3 Wewe unapenda uovu kuliko wema na udanganifu kuliko kuongea haki. (Selah)
Thou lovest evil more than good; falsehood rather than speaking righteousness. (Selah)
4 Wewe hupenda maneno ambayo huwaumiza wengine, wewe ulimi mdanganyifu.
Thou lovest all devouring words, the deceitful tongue.
5 Vivyo hivyo Mungu atakuadhibu wewe milele; yeye atakuchukua na kukuondoa katika hema yako na kukung'oa katika ardhi ya uhai. (Selah)
God will likewise break thee for ever, He will take thee up, and pluck thee out of thy tent, and root thee out of the land of the living. (Selah)
6 Wenye haki pia wataona na kuogopa; watamcheka na kusema,
The righteous also shall see, and fear, and shall laugh at him:
7 “Tazama, huyu ni mtu ambaye hakumfanya Mungu kuwa kimbilio lake la usalama, bali aliamini katika wingi wa mali zake, naye alikuwa na nguvu alipowaharibu wengine.”
'Lo, this is the man that made not God his stronghold; but trusted in the abundance of his riches, and strengthened himself in his wickedness.'
8 Lakini kwangu mimi, niko kama mti bora wa mzeituni katika nyumba ya Mungu; Nami nitaamini uaminifu wa agano la Mungu milele na milele.
But as for me, I am like a leafy olive-tree in the house of God; I trust in the mercy of God for ever and ever.
9 Nitakushukuru wewe daima kwa uliyo tenda. Nitalisubiri jina lako, kwa sababu ni zuri, uweponi mwa wantu wako wa kimungu.
I will give Thee thanks for ever, because Thou hast done it; and I will wait for Thy name, for it is good, in the presence of Thy saints.

< Zaburi 52 >