< Zaburi 50 >

1 Mungu, Mwenye nguvu, Yahwe, amenena naye aliita nchi toka mawio ya jua mpaka machweo yake.
A Psalm of Asaph. God, [even] God, the LORD, hath spoken, and called the earth from the rising of the sun unto the going down thereof.
2 Tokea Sayuni, Mungu ameangaza, ukamilifu wa uzuri.
Out of Zion, the perfection of beauty, God hath shined forth.
3 Mungu wetu huja naye hakai kimya; mbele yake moto hula, na kuna dhoruba kubwa karibu naye.
Our God shall come, and shall not keep silence: a fire shall devour before him, and it shall be very tempestuous round about him.
4 Yeye huziita mbingu zilizo juu na nchi ili kwamba aweze kuwahukumu watu wake:
He shall call to the heavens above, and to the earth, that he may judge his people:
5 Kwa pamoja kusanyikeni waaminifu wangu kwangu, wale waliofanya nami agano kwa sadaka.”
Gather my saints together unto me; those that have made a covenant with me by sacrifice.
6 Mbingu zitatangaza haki yake, kwa maana Mungu mwenyewe ndiye jaji. Serah
And the heavens shall declare his righteousness; for God is judge himself. (Selah)
7 Sikilizeni, watu wangu, nami nitazungumza; mimi ni Mungu, Mungu wenu.
Hear, O my people, and I will speak; O Israel, and I will testify unto thee: I am God, [even] thy God.
8 Sitawakaripia ninyi kwa ajili ya sadaka zenu; sadaka zenu za kuteketeza ziko nami siku zote.
I will not reprove thee for thy sacrifices; and thy burnt offerings are continually before me.
9 Sitachukua ng'ombe katika nyumba yenu, wala beberu katika mazizi yenu.
I will take no bullock out of thy house, nor he-goats out of thy folds.
10 Kwa maana kila mnyama wa msituni ni wangu, nao ng'ombe kwenye milima elfu ni wangu.
For every beast of the forest is mine, and the cattle upon a thousand hills.
11 Ninawajua ndege wa mlimani, na wanyama pori katika shamba ni wangu.
I know all the fowls of the mountains: and the wild beasts of the field are mine.
12 Kama ningekuwa na njaa, nisingewaambia ninyi; maana ulimwengu ni wangu, na vyote vilivyomo.
If I were hungry, I would not tell thee: for the world is mine, and the fulness thereof.
13 Je! sitakula nyama ya ngombe na kunywa damu ya mbuzi?
Will I eat the flesh of bulls, or drink the blood of goats?
14 Mtoleeni Mungu sadaka za shukurani, na mlipe viapo vyenu kwa Aliye Juu.
Offer unto God the sacrifice of thanksgiving; and pay thy vows unto the Most High:
15 Mniite katika siku ya shida; nami nitawaokoa
And call upon me in the day of trouble; I will deliver thee, and thou shalt glorify me.
16 Lakini kwa waovu Mungu anasema, “Inawahusu nini kuitangaza hali yangu, kwamba ninyi mmeliweka agano langu mdomoni mwenu,
But unto the wicked God saith, What hast thou to do to declare my statutes; and that thou hast taken my covenant in thy mouth?
17 wakati ninyi mnayachukia maelekezo na mnayatupa maneno yangu?
Seeing thou hatest instruction, and castest my words behind thee.
18 Mumuanapo mwizi, ninyi hukubaliana naye; ninyi na mnashirikiana na wale wafanyao uasherati.
When thou sawest a thief, thou consentedst with him, and hast been partaker with adulterers.
19 Mwautoa mdomo wenu kwa mabaya, huelezea udanganyifu.
Thou givest thy mouth to evil, and thy tongue frameth deceit.
20 Mnakaa na kuongea dhidi ya ndugu yenu; na kukashfu mwana wa mama yenu.
Thou sittest and speakest against thy brother; thou slanderest thine own mother’s son.
21 Mmefanya mambo haya, lakini nimekaa kimya, hivyo mlidhani kuwa ni mtu flani nilliye kama ninyi mlivyo. Lakini nitawakaripia ninyi na kuwafunua, mbele ya macho yenu, mambo yote miliyofanya.
These things hast thou done, and I kept silence; thou thoughtest that I was altogether such an one as thyself: [but] I will reprove thee, and set [them] in order before thine eyes.
22 Mlitilie maanani hili, ninyi mnao msahau Mungu, vinginevyo nitawakata ninyi vipande vipande, na hatakuwepo yeyote wakuja kuwasaidia!
Now consider this, ye that forget God, lest I tear you in pieces, and there be none to deliver:
23 Yule atoaye sadaka ya shukurani hunitukuza, na yeyote apangaye njia zake katika namna iliyo sahihi nitamuonesha wokovu wa Mungu.”
Whoso offereth the sacrifice of thanksgiving glorifieth me; and to him that ordereth his conversation [aright] will I shew the salvation of God.

< Zaburi 50 >