< Zaburi 46 >

1 Mungu kwetu ni kimbilio la usalama na nguvu, upatikanao tele wakati wa mateso.
To the Overseer. — By sons of Korah. 'For the Virgins.' — A song. God [is] to us a refuge and strength, A help in adversities found most surely.
2 Hivyo hatutaogopa, hata kama dunia italazimika kubadilika, hata kama milima italazimika kutetemeka na kuangukia kwenye mtima wa bahari, hata kama maji yatavuma kwa kishindo kikuu,
Therefore we fear not in the changing of earth, And in the slipping of mountains Into the heart of the seas.
3 hata kama milima itatetemeka kwa vurugu ya maji. (Selah)
Roar — troubled are its waters, Mountains they shake in its pride. (Selah)
4 Kuna mto, mikondo yake huufanya mji wa Mungu kufurahi, mahali patakatifu pa hema ya Aliye Juu.
A river — its rivulets rejoice the city of God, Thy holy place of the tabernacles of the Most High.
5 Mungu yuko katikati yake; naye hatasogezwa; Mungu atamsaidia, naye atafanya hivyo asubuhi na mapema.
God [is] in her midst — she is not moved, God doth help her at the turn of the morn!
6 Mataifa yalikasirika na falme zikataharuki; yeye alipaza sauti yake, na nchi ikayeyuka.
Troubled have been nations, Moved have been kingdoms, He hath given forth with His voice, earth melteth.
7 Yahwe wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. (Selah)
Jehovah of Hosts [is] with us, A tower for us [is] the God of Jacob. (Selah)
8 Njoni, mtazame matendo ya Yahwe, uharibifu alioufanya juu ya nchi.
Come ye, see the works of Jehovah, Who hath done astonishing things in the earth,
9 Anaisitisha vita kwenye nchi; yeye anauvunja upinde na kuikata vipande vipande mishale; anazichoma ngao.
Causing wars to cease, Unto the end of the earth, the bow he shivereth, And the spear He hath cut asunder, Chariots he doth burn with fire.
10 Mkae kimya na mjue kuwa mimi ni Mungu; nitainuliwa juu ya nchi.
Desist, and know that I [am] God, I am exalted among nations, I am exalted in the earth.
11 Mungu wa majeshi yuko pamoja nasi; Mungu wa Yakobo ni kimbilio letu la usalama. Serah
Jehovah of hosts [is] with us, A tower for us [is] the God of Jacob! (Selah)

< Zaburi 46 >