< Zaburi 34 >

1 Nitamsifu Yahwe wakati wote, siku zote sifa zake zitakuwa mdomoni mwangu.
Davidi, cum immutavit vultum suum coram Achimelech, et dimisit eum et abiit. Benedicam Dominum in omni tempore: semper laus eius in ore meo.
2 Nitamsifu Yahwe! walio onewa wasikie na kufurahi.
In Domino laudabitur anima mea: audiant mansueti, et lætentur.
3 Msifuni Yahwe pamoja nami, kwa pamoja tuliinue jina lake.
Magnificate Dominum mecum: et exaltemus nomen eius in idipsum.
4 Nilimuomba Yahwe msaada naye akanijibu, akanipa ushindi juu ya hofu yangu yote.
Exquisivi Dominum, et exaudivit me: et ex omnibus tribulationibus meis eripuit me.
5 Wale wanao mtazama yeye wana furaha, na nyuso zao hazina aibu.
Accedite ad eum, et illuminamini: et facies vestræ non confundentur.
6 Huyu mtu aliye onewa alilia na Yahwe akamsikia na kumuokoa kwenye matatizo yake yote.
Iste pauper clamavit, et Dominus exaudivit eum: et de omnibus tribulationibus eius salvavit eum.
7 Malaika wa Yahwe huweka kambi wakiwazunguka wale wanao muogopa yeye na kuwaokoa.
Immittet angelus Domini in circuitu timentium eum: et eripiet eos.
8 Onjeni muone Yahwe ni mzuri. Amebarikiwa mtu yule ambaye Yahwe ni kimbilio lake.
Gustate, et videte quoniam suavis est Dominus: beatus vir, qui sperat in eo.
9 Muogopeni Yahwe, ninyi watu watakatifu wake. Hakuna kupungukikwa kwa wale wanao mhofu yeye.
Timete Dominum omnes sancti eius: quoniam non est inopia timentibus eum.
10 Simba wadogo wakati mwingine hukosa chakula na kuteseka kwa njaa, bali wale wamtafutao Yahwe hawatapungukiwa chochote kilicho kizuri.
Divites eguerunt et esurierunt: inquirentes autem Dominum non minuentur omni bono.
11 Njoni, wana, mnisikilize mimi. nitawafundisha ninyi hofu ya Yahwe.
Venite filii, audite me: timorem Domini docebo vos.
12 Mtu nani aliyepo ambaye anatamani maisha na anapenda kuwa na siku nyingi, ili kwamba aweze kuona vizuri?
Quis est homo qui vult vitam: diligit dies videre bonos?
13 Hivyo uepushe ulimi wako na uovu na uilinde midomo yako kuongea uongo.
Prohibe linguam tuam a malo: et labia tua ne loquantur dolum.
14 Uache uovu na utende mema. Uitafute amani na kuiendea amani.
Diverte a malo, et fac bonum: inquire pacem, et persequere eam.
15 Macho ya Yahwe yako kwenye haki na masikio yake huelekea kulia kwao.
Oculi Domini super iustos: et aures eius in preces eorum.
16 Uso wa Yahwe uko kinyume na wale watendao uovu, kuikatilia mbali kumbukumbu yao duniani.
Vultus autem Domini super facientes mala: ut perdat de terra memoriam eorum.
17 Wenye haki hulia na Yahwe husikia na kuwaokoa kwenye matatizo yao yote.
Clamaverunt iusti, et Dominus exaudivit eos: et ex omnibus tribulationibus eorum liberavit eos.
18 Yahwe yu karibu nao waliovunjika moyo, naye huwaokoa waliogandamizwa rohoni.
Iuxta est Dominus iis, qui tribulato sunt corde: et humiles spiritu salvabit.
19 Mateso ya wenye haki ni mengi, bali Yahwe huwaokoa nayo yote.
Multæ tribulationes iustorum: et de omnibus his liberabit eos Dominus.
20 Yeye huitunza mifupa yake yote, hakuna hata mmoja wao utavunjika.
Custodit Dominus omnia ossa eorum: unum ex his non conteretur.
21 Uovu utawauwa waovu. Wale wachukiao haki watahukumiwa.
Mors peccatorum pessima: et qui oderunt iustum delinquent.
22 Yahwe huokoa maisha ya watumishi wake. Hakuna atakaye hukumiwa hata mmoja atafutaye usalama katika yeye.
Redimet Dominus animas servorum suorum: et non delinquent omnes qui sperant in eo.

< Zaburi 34 >