< Zaburi 29 >

1 Mpeni sifa Yahwe, enyi wana wa Mungu! Mpeni sifa Yahwe kwa ajili ya utukufu wake na nguvu.
A Psalm of David. Ascribe to Jehovah, ye sons of the mighty, Ascribe to Jehovah honour and strength.
2 Mpeni Yahwe utukufu ambao jina lake linastahili. Mpigieni magoti Yahwe katika mapambo ya utakatifu.
Ascribe to Jehovah the honour of His name, Bow yourselves to Jehovah, In the beauty of holiness.
3 Sauti ya Yahwe imesikika zaidi ya maji; Mungu wa radi ya utukufu, radi yaYahwe i juu ya maji mengi.
The voice of Jehovah [is] on the waters, The God of glory hath thundered, Jehovah [is] on many waters.
4 Sauti ya Yahwe ina nguvu; sauti ya Yahwe ni kuu.
The voice of Jehovah [is] with power, The voice of Jehovah [is] with majesty,
5 Sauti ya Yahwe huivunja mierezi; Yahwe huivunja vipande vipande mierezi ya Lebanon.
The voice of Jehovah [is] shivering cedars, Yea, Jehovah shivers the cedars of Lebanon.
6 Yeye huifanya Lebanoni kuruka kama ndama wa ng'ombe na Sirioni kama mwana wa nyati.
And He causeth them to skip as a calf, Lebanon and Sirion as a son of Reems,
7 Sauti ya Yahwe hutoa miale ya moto.
The voice of Jehovah is hewing fiery flames,
8 Sauti ya Yahwe hutetemesha Jangwa; Yahwe hutetemesha jangwa la Kadeshi.
The voice of Jehovah paineth a wilderness, Jehovah paineth the wilderness of Kadesh.
9 Sauti ya Yahwe huufanya miti mikubwa kutikisika na huipukutisha misitu. Kila mmoja katika hekalu lake husema, “Utukufu!”
The voice of Jehovah paineth the oaks, And maketh bare the forests, And in His temple every one saith, 'Glory.'
10 Yahwe hukaa kama mfalme juu ya mafuriko; Yahwe hukaa kama mfalme milele.
Jehovah on the deluge hath sat, And Jehovah sitteth king — to the age,
11 Yahwe huwatia nguvu watu wake; Yahwe huwa bariki watu wake na amani.
Jehovah strength to his people giveth, Jehovah blesseth His people with peace!

< Zaburi 29 >