< Zaburi 25 >

1 Kwako, Yahwe, nayainua maisha yangu!
[A Psalm] of David. Unto thee, O LORD, do I lift up my soul.
2 Mungu wangu, ninaamini katika wewe. Usiniache niaibishwe; usiwaache maadui zangu wafurahie ushindi wao kwangu.
O my God, in thee have I trusted, let me not be ashamed; let not mine enemies triumph over me.
3 Asiaibishwe mtu yeyote anaye kutumaini bali waaibishwe wale watendao hila bila sababu!
Yea, none that wait on thee shall be ashamed: they shall be ashamed that deal treacherously without cause.
4 Unijulishe njia zako, Yahwe; unifundishe njia zako.
Shew me thy ways, O LORD; teach me thy paths.
5 Uniongoze kwenye kweli yako na unifundishe, kwa kuwa wewe ni Mungu wa wokovu wangu; ninakutumainia wewe siku zote za maisha yangu.
Guide me in thy truth, and teach me; for thou art the God of my salvation; on thee do I wait all the day.
6 Kumbuka, Yahwe, matendo yako ya huruma na uaminifu wa agano lako; kwa kuwa vimekuwapo siku zote.
Remember, O LORD, thy tender mercies and thy lovingkindnesses; for they have been ever of old.
7 Usizikumbuke dhambi za ujana wangu wala uasi wangu; Uniweke akilini mwako pamoja na uaminifu wa agano kwa zababu ya uzuri wa wako, Yahwe!
Remember not the sins of my youth, nor my transgressions: according to thy lovingkindness remember thou me, for thy goodness’ sake, O LORD.
8 Yahwe ni mzuri na mwenye haki; kwa hiyo yeye huwafundisha njia mwenye dhambi.
Good and upright is the LORD: therefore will he instruct sinners in the way.
9 Yeye huwaelekeza wanyenyekevu kwa kile kilicho sahihi na yeye huwafundisha wao njia yake.
The meek will he guide in judgment: and the meek will he teach his way.
10 Njia zote za Yahwe ni za upendo wa kudumu na niaminifu kwa wote wanao tunza agano na maagizo ya amri zake.
All the paths of the LORD are lovingkindness and truth unto such as keep his covenant and his testimonies.
11 Kwa ajili ya jina lako, Yahwe, unisamehe dhambi zangu, kwa kuwa ni nyingi mno.
For thy name’s sake, O LORD, pardon mine iniquity, for it is great.
12 Ni nani ambaye anamuogopa Yahwe? Bwana atamfundisha yeye katika njia ambayo anapaswa kuichagua.
What man is he that feareth the LORD? him shall he instruct in the way that he shall choose.
13 Maisha yake yataenenda katika uzuri; na uzao wake utairithi nchi.
His soul shall dwell at ease; and his seed shall inherit the land.
14 Urafiki wa Yahwe ni kwa ajili ya wale wanao mheshimu yeye, naye hulifanya agano lake lijulikane kwao.
The secret of the LORD is with them that fear him; and he will shew them his covenant.
15 Siku zote macho yangu yanamtazama Yahwe, kwa kuwa yeye ataifungua miguu yangu kwenye nyavu.
Mine eyes are ever toward the LORD; for he shall pluck my feet out of the net.
16 Unigeukie mimi na unihurumie; kwa maana niko peke yangu na niliye matesoni.
Turn thee unto me, and have mercy upon me; for I am desolate and afflicted.
17 Maumivu ya moyo wangu yameongezeka; uniondoe katika dhiki hii!
The troubles of my heart are enlarged: O bring thou me out of my distresses.
18 Tazama mateso yangu na taabu yangu; unisamehe dhambi zangu zote.
Consider mine affliction and my travail; and forgive all my sins.
19 Ona maadui zangu, kwa maana ni wengi; wananichukia kwa chuki ya kikatili.
Consider mine enemies, for they are many; and they hate me with cruel hatred.
20 Uyalinde maisha yangu na uniokoe; usiniache niaibishwe, Kwa kuwa kwako nakimbilia usalama!
O keep my soul, and deliver me: let me not be ashamed, for I put my trust in thee.
21 Uadilifu na unyofu vinihifadhi, kwa kuwa nina kutumainia wewe.
Let integrity and uprightness preserve me, for I wait on thee.
22 Mungu, uiokoe Israeli, na shida yake yote!
Redeem Israel, O God, out of all his troubles.

< Zaburi 25 >