< Zaburi 24 >

1 Nchi ni ya Yahwe, na vyote viijazavyo, dunia, na wote wakaao ndani yake.
Of David. A psalm. The earth is the Lord’s and all that it holds, the world and those who live in it.
2 Kwa kuwa yeye aliianzisha juu ya bahari na kuiimarisha juu ya mito.
For he founded it on the seas, and on the floods he sustains it.
3 Ni nani atakaye panda mlima wa Yahwe? Ni nani atakaye simama patakatifu pake?
Who may ascend the hill of the Lord? Who may stand in his holy place?
4 Yeye ambaye ana mikono misafi na moyo safi; ambaye hajauinua uongo, na haja apa kiapo ili kudanganya.
The clean of hands, the pure of heart, who sets not their heart upon sinful things, nor swears with intent to deceive:
5 Yeye atapokea baraka kutoka kwa Yahwe na haki kutoka kwa Mungu wa wokovu wake.
they win from the Lord a blessing: God is their champion and savior.
6 Kizazi cha wale wamtafutao Mungu ni kama hiki, wale ambao wanautafuta uso wa Mungu wa Yakobo.
Such must be those who resort to him, and seek the face of the God of Jacob. (Selah)
7 Inueni vichwa vyenu, ninyi malango; muinuliwe juu, milango ya milango ya kudumu, ili kwamba Mfalme wa utukufu aweze kuingia!
Lift high your heads, you gates – Higher, you ancient doors; welcome the glorious king.
8 Huyu Mfalme wa utukufu ni nani? Yahwe, mwenye nguvu na uweza; Yahwe, mwenye uweza katika vita.
“Who is the glorious king?” “The Lord strong and heroic, the Lord heroic in battle.”
9 Inueni vichwa vyenu, ninyi malango; muinuliwe juu, milango ya kudumu, ili kwamba Mfalme wa utukufu aweze kuingia!
Lift high your heads, you gates – Higher, you ancient doors; welcome the glorious king.
10 Huyu Mfalme wa utukufu ni nani? Yahwe wa majeshi, yeye ni Mfalme wa utukufu.
“Who is the glorious king?” “The Lord, the God of hosts, he is the glorious king.” (Selah)

< Zaburi 24 >