< Zaburi 23 >

1 Yahwe ni mchungaji wangu; sita pungukiwa na kitu.
Yavé es mi Pastor. Nada me faltará.
2 Yeye hunilaza katika majani mabichi; huniongoza kando ya maji matulivu.
En lugares de tiernos prados me hace descansar. Junto a aguas de reposo me conduce.
3 Yeye huurejesha uhai wangu; huniongoza katika njia iliyo sahihi kwa ajili ya jina lake.
Restaura mi alma. Me guía por sendas de justicia por amor a su Nombre.
4 Hata ijapokuwa nikipita katika bonde la uvuli na giza nene, sitaogopa kudhurika kwa kuwa wewe uko pamoja nami; fimbo yako na gongo lako vya nifariji.
Aunque ande por el valle de la sombra de muerte, No temeré algún mal, Porque Tú estás conmigo. Tu vara y tu cayado me confortan.
5 Wewe waandaa meza mbele yangu katika uwepo wa maadui zangu; umenipaka mafuta kichwa changu na kikombe changu kinafurika.
Aderezas mesa delante de mí en presencia de mis adversarios. Unges mi cabeza con aceite. Mi copa rebosa.
6 Hakika wema na uaminifu wa agano vitaniandama siku zote za maisha yangu; nami nitaishi katika nyumba ya Yahwe milele!
Ciertamente el bien y la misericordia me escoltarán todos los días de mi vida, Y en la Casa de Yavé moraré por largos días.

< Zaburi 23 >