< Zaburi 142 >

1 Kwa sauti yangu namlilia Yahwe anisaidie; kwa sauti yangu naomba kwa ajili ya neema ya Yahwe.
I cry with my voice to Adonai. With my voice, I ask Adonai for mercy.
2 Namwaga malalamiko yangu mbele zake; ninamwambia shida zangu.
I pour out my complaint before him. I tell him my troubles.
3 Roho yangu inapokuwa dhaifu ndani yangu, wewe unajua mapito yangu. Kwenye njia niipitayo wamenifichia mtego.
When my spirit was overwhelmed within me, you knew my route. On the path in which I walk, they have hidden a snare for me.
4 Natazama kulia kwangu na sioni yeyote anayenijali. Sina pa kukimbilia; hakuna anayejali kuhusu uhai wangu.
Look on my right, and see; for there is no one who is concerned for me. Refuge has fled from me. No one cares for my soul.
5 Nilikuita wewe, Yahwe; nikasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.
I cried to you, Adonai. I said, “You are my refuge, my portion in the land of the living.”
6 Sikia kuita kwangu, maana nimeshushwa chini sana; uniokoe dhidi ya watesi wangu, maana wana nguvu kuliko mimi.
Listen to my cry, for I am in desperate need. Deliver me from my persecutors, For they are stronger than me.
7 Uitoe nafsi yangu kifungoni ili niweze kulishukuru jina lako. Wenye haki watakusanyika karibu nami kwa sababu umekuwa mwema kwangu.”
Bring my soul out of prison, that I may yadah ·extend hands in thankful praise· to your name. The upright will surround me, for you will be good to me.

< Zaburi 142 >