< Zaburi 141 >

1 Ee Yahwe, ninakulilia wewe; uje upesi kwangu. Unisikilize nikuitapo.
Adonai, I have called on you. Come to me quickly! Listen to my voice when I call to you.
2 Maombi yangu na yawe kama uvumba mbele zako; mikono yangu iliyoinuliwa na iwe kama dhabihu ya jioni.
Let my prayer be set before you like incense; the lifting up of my hands like the evening sacrifice.
3 Ee Yahwe, uweke mlinzi kinywani mwangu; mngojezi malangoni pa midomo yangu.
Set a watch, Adonai, before my mouth. Keep the door of my lips.
4 Usiruhusu tamaa ya moyo wangu kutamani uovu wowote wala kushiriki katika matendo ya dhambi na watu waishio maovuni. Nisile vyakula vyao vya anasa.
Don’t incline my heart to any evil thing, to practice deeds of wickedness with men who work iniquity. Don’t let me eat of their delicacies.
5 Mwenye haki na anipige; nao utakuwa ni wema kwangu. Anirudi; itakuwa kama mafuta kichwani pangu; kichwa changu na kisikatae kupokea. Lakini maombi yangu siku zote yatakuwa dhidi ya matendo yao mauvu.
Let the upright strike me, it is kindness; let him reprove me, it is like oil on the head; don’t let my head refuse it; Yet my prayer is always against evil deeds.
6 Viongozi wao watatupwa chini toka juu mlimani; watayasikia maneno yangu kuwa ni matamu.
Their judges are thrown down by the sides of the rock. They will sh'ma ·hear obey· my words, for they are well spoken.
7 Watalazimika kusema, “Kama vile jembe moja livunjapo ardhi, hivyo mifupa yetu imesambaratishwa kinywani pa kuzimu.” (Sheol h7585)
“As when one plows and breaks up the earth, our bones are scattered at the mouth of Sheol ·Place of the dead·.” (Sheol h7585)
8 Hakika macho yangu yanakutazama wewe, Yahwe, Bwana; katika wewe napata kimbilio; usiiache nafsi yangu.
For my eyes are on you, Adonai, the Lord. In you, I take refuge. Don’t leave my soul destitute.
9 Unilinde dhidi ya mitego waliyoiweka kwa ajili yangu, na matanzi yao watendao maovu.
Keep me from the snare which they have laid for me, from the traps of the workers of iniquity.
10 Waovu na waangukie kwenye nyavu zao wenywe pindi mimi nitorokapo.
Let the wicked fall together into their own nets, while I pass by.

< Zaburi 141 >