< Zaburi 138 >

1 Nitakushukuru kwa moyo wangu wote; mbele ya miungu nitakuimbia sifa.
I will yadah ·extend hands in thankful praise· to with my whole heart. Before the deities, I will sing zahmar ·musical praise· to you.
2 Nitasujundu mbele ya hekalu lako takatifu na kulishukuru jina lako kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na kwa uaminifu wako. Umelifanya muhimu zaidi neno lako na jina lako kuliko kitu chochote.
I will bow down toward your holy temple, and yadah ·extend hands in thankful praise· to your Name for your cheshed ·loving-kindness· and for your truth; for you have exalted your Name and your Word above all.
3 Siku ile niliyo kuita, ulinijibu; ulinitia moyo na kuitia nguvu nafsi yangu.
In the day that I called, you answered me. You encouraged me with strength in my soul.
4 Wafalme wote wa nchi watakushukuru wewe, Yahwe, maana watasikia maneno kutoka kinywani mwako.
All the kings of the earth will yadah ·extend hands in thankful praise· to Adonai, for they have sh'ma ·heard obeyed· the words of your mouth.
5 Hakika, wataimba kuhusu matendo ya Yahwe, kwa kuwa utukufu wa Yahwe ni mkuu.
Yes, they will sing of the ways of Adonai; for great is the kavod Yahweh ·weighty glory of He sustains breathing·.
6 Maana ingawa Yahwe yuko juu, lakini anawajali wanyenyekevu, lakini hawatambui wenye majivuno.
For though Adonai is high, yet he looks after the lowly; but the proud, he knows from afar.
7 Nijapopita katikati ya hatari, wewe utauhifadhi uhai wangu; utanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, na mkono wako wa kuume utaniokoa.
Though I walk in the middle of trouble, you will revive me. You will stretch out your hand against the wrath of my enemies. Your right hand will save me.
8 Yahwe yuko pamoja nami hadi mwisho; uaminifu wa agano lako, Yahwe, wadumu milele. Usiwaache wale ambao mikono yako imewaumba.
Adonai will fulfill that which concerns me; your cheshed ·loving-kindness·, Adonai, endures forever. Don’t forsake the works of your own hands.

< Zaburi 138 >