< Zaburi 135 >

1 Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
Halleluyah ·praise Yah·! Praise Adonai’s name! Praise him, you servants of Adonai,
2 ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
you who stand in Adonai’s house, in the courts of our God’s house.
3 Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
Halleluyah ·praise Yah·, for Adonai is good. Sing zahmar ·musical praise· to his name, for that is pleasant.
4 Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
For Yah has chosen Jacob [Supplanter] for himself; Israel [God prevails] for his own segulah ·special treasure·.
5 Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
For I know that Adonai is great, that our Lord is above all deities.
6 Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
Whatever Adonai pleased, that he has done, in heaven and in earth, in the seas and in all deeps;
7 Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
who causes the clouds to rise from the ends of the earth; who makes lightnings with the rain; who brings the wind out of his treasuries;
8 Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
Who struck the firstborn of Egypt [Abode of slavery], both of man and animal;
9 Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Who sent signs and wonders into the middle of you, Egypt [Abode of slavery], on Pharaoh, and on all his servants;
10 Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
who struck many nations, and killed mighty kings,
11 Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
Sihon king of the Amorites [Descendants of Talkers], Og king of Bashan, and all the kingdoms of Canaan [Humbled],
12 Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
and gave their land for a heritage, a heritage to Israel [God prevails], his people.
13 Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
Your name, Adonai, endures forever; your renown, Adonai, throughout all generations.
14 Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
For Adonai will judge his people, and have compassion on his servants.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
The idols of the nations are silver and gold, the work of men’s hands.
16 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
They have mouths, but they can’t speak. They have eyes, but they can’t see.
17 zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
They have ears, but they can’t hear; neither is there any breath in their mouths.
18 Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
Those who make them will be like them; yes, everyone who trusts in them.
19 Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
House of Israel [God prevails], praise Adonai! House of Aaron [Light-bringer], praise Adonai!
20 Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
House of Levi [United with], praise Adonai! You who fear Adonai, praise Adonai!
21 Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.
Blessed be Adonai from Zion [Mountain ridge, Marking], Who dwells at Jerusalem [City of peace]. Halleluyah ·praise Yah·!

< Zaburi 135 >