< Zaburi 13 >

1 Mpaka lini, Yahweh, utaendelea kunisahau? Ni kwa muda gani utauficha uso wako nisiuone?
To the Overseer. — A Psalm of David. Till when, O Jehovah, Dost Thou forget me? — for ever? Till when dost Thou hide Thy face from me?
2 Ni kwa muda gani nitalazimika kuhofu na kuhuzunika moyoni mwangu kila siku? Ni kwa muda gani adui zangu watanishida?
Till when do I set counsels in my soul? Sorrow in my heart daily? Till when is mine enemy exalted over me?
3 Unitazame na unijibu, Yahwe Mungu wangu! Nipe mwanga machoni pangu, vinginevyo nitalala katika mauti.
Look attentively; Answer me, O Jehovah, my God, Enlighten mine eyes, lest I sleep in death,
4 Usimuache adui yangu aseme, “Nimemshinda huyu,” ili kwamba asiweze kusema, “Nimemtawala adui yangu;” la sivyo, maadui zangu watafurahia nitakapo shushwa chini.
Lest mine enemy say, 'I overcame him,' Mine adversaries joy when I am moved.
5 Lakini nimeamini katika uaminifu wa agano lako; moyo wangu wafurahia katika wokovu wako.
And I, in Thy kindness I have trusted, Rejoice doth my heart in Thy salvation.
6 Nitamuimbia Yahwe kwa kuwa ameniganga kwa ukarimu kabisa.
I do sing to Jehovah, For He hath conferred benefits upon me!

< Zaburi 13 >