< Zaburi 129 >

1 “Mara nyingi tangu ujana wangu wamekuwa wakinishambulia,” Israeli na iseme.
[the] song of The ascents much people have opposed me since youth my let it say please Israel.
2 “Mara nyingi tangu ujana wangu wamekuwa wakinishambulia, lakini hawajanishinda.
Much people have opposed me since youth my also not they have prevailed to me.
3 Wakulima wamekuwa wakilima mgonngoni kwangu; wametengeneza matuta yao marefu.
On back my they have plowed plowmen they have made long (furrows their. *QK)
4 Yahwe ni mwenye haki; amezikata kamba za waovu.”
Yahweh [is] righteous he has cut off [the] rope of wicked [people].
5 Wote waaibishwe na kurudishwa nyuma, wale wachukiao Sayuni.
May they be ashamed and they may be turned back backward all [those who] hate Zion.
6 Na wawe kama nyasi juu ya paa ambayo hunyauka kabla hayajakua,
May they be like [the] grass of roofs that before it has shot up it has withered.
7 ambayo hayawezi kujaza mkono wa mvunaji wala kifua cha mfunga miganda.
That not he has filled hand his a reaper and bosom his [one who] binds sheaves.
8 Wale wapitao karibu wasiseme, “Baraka za Mungu na ziwe juu yako; Tunakubariki katika jina la Yahwe.”
And not they say - those [who] pass by [the] blessing of Yahweh [be] to you we bless you in [the] name of Yahweh.

< Zaburi 129 >