< Zaburi 129 >

1 “Mara nyingi tangu ujana wangu wamekuwa wakinishambulia,” Israeli na iseme.
Many times they have afflicted me from my youth up. Let Israel [God prevails] now say,
2 “Mara nyingi tangu ujana wangu wamekuwa wakinishambulia, lakini hawajanishinda.
many times they have afflicted me from my youth up, yet they have not prevailed against me.
3 Wakulima wamekuwa wakilima mgonngoni kwangu; wametengeneza matuta yao marefu.
The plowers plowed on my back. They made their furrows long.
4 Yahwe ni mwenye haki; amezikata kamba za waovu.”
Adonai is righteous. He has cut apart the cords of the wicked.
5 Wote waaibishwe na kurudishwa nyuma, wale wachukiao Sayuni.
Let them be disappointed and turned backward, all those who hate Zion [Mountain ridge, Marking].
6 Na wawe kama nyasi juu ya paa ambayo hunyauka kabla hayajakua,
Let them be as the grass on the housetops, which withers before it grows up;
7 ambayo hayawezi kujaza mkono wa mvunaji wala kifua cha mfunga miganda.
with which the reaper does not fill his hand, nor he who binds sheaves, his bosom.
8 Wale wapitao karibu wasiseme, “Baraka za Mungu na ziwe juu yako; Tunakubariki katika jina la Yahwe.”
Neither do those who go by say, “The blessing of Adonai be on you. We bless you in Adonai’s name.”

< Zaburi 129 >