< Zaburi 115 >

1 Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
Nicht uns, Jehovah, nicht uns, sondern Deinem Namen gib Herrlichkeit, um Deiner Barmherzigkeit, um Deiner Wahrheit willen!
2 Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
Warum sollen die Völkerschaften sagen: Wo ist nun ihr Gott?
3 Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
Aber unser Gott ist in den Himmeln, Er kann tun, wozu Er Lust hat.
4 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Ihre Götzenbilder sind Silber und Gold, gemacht von den Händen des Menschen.
5 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
Einen Mund haben sie und reden nicht, Augen haben sie und sehen nicht;
6 zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
Ohren haben sie und hören nicht, eine Nase haben sie und riechen nicht;
7 Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
Ihre Hände, und sie tasten nicht, ihre Füße, und sie gehen nicht, sie sprechen nicht aus ihrer Kehle.
8 Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
Wie sie sind die, so sie machen, jeder, der auf sie vertraut.
9 Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
Israel, vertraue auf Jehovah! Ihr Beistand und ihr Schild ist Er.
10 Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
Haus Aharons, vertrauet auf Jehovah; ihr Beistand und ihr Schild ist Er.
11 Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
Ihr, die ihr Jehovah fürchtet, vertrauet auf Jehovah; ihr Beistand und ihr Schild ist Er.
12 Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
Jehovah gedenkt unser, Er segnet: Er segnet das Haus Israel, Er segnet das Haus Aharons.
13 Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
Er segnet die, so Jehovah fürchten, die Kleinen mit den Großen.
14 Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
Jehovah wird zu euch hinzutun, zu euch und zu euren Söhnen.
15 Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
Gesegnet seid ihr dem Jehovah, Der Himmel und Erde gemacht.
16 Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
Die Himmel, die Himmel sind Jehovahs, und die Erde gab Er den Söhnen des Menschen.
17 Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
Die Toten loben nicht Jah, noch alle, die zur Stille hinabfahren.
18 bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.
Wir aber segnen Jah von nun an und bis in Ewigkeit. Hallelujah!

< Zaburi 115 >