< Zaburi 115 >

1 Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
Not unto us, O LORD, not unto us, but unto thy name give glory, for thy mercy, and for thy truth’s sake.
2 Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
Wherefore should the nations say, Where is now their God?
3 Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
But our God is in the heavens: he hath done whatsoever he pleased.
4 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Their idols are silver and gold, the work of men’s hands.
5 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
They have mouths, but they speak not; eyes have they, but they see not;
6 zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
They have ears, but they hear not; noses have they, but they smell not;
7 Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
They have hands, but they handle not; feet have they, but they walk not; neither speak they through their throat.
8 Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
They that make them shall be like unto them; yea, every one that trusteth in them.
9 Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
O Israel, trust thou in the LORD: he is their help and their shield.
10 Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
O house of Aaron, trust ye in the LORD: he is their help and their shield.
11 Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
Ye that fear the LORD, trust in the LORD: he is their help and their shield.
12 Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
The LORD hath been mindful of us; he will bless [us]: he will bless the house of Israel; he will bless the house of Aaron.
13 Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
He will bless them that fear the LORD, both small and great.
14 Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
The LORD increase you more and more, you and your children.
15 Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
Blessed are ye of the LORD, which made heaven and earth.
16 Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
The heavens are the heavens of the LORD; but the earth hath he given to the children of men.
17 Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
The dead praise not the LORD, neither any that go down into silence;
18 bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.
But we will bless the LORD from this time forth and for evermore. Praise ye the LORD.

< Zaburi 115 >