< Zaburi 115 >

1 Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
Not to us, Lord, not to us, but to your name give glory, for your kindness’ and faithfulness’ sake.
2 Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
Why should the heathen say, “Where is now their God?”
3 Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
Our God he is in heaven; whatever he wishes, he does.
4 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Their idols are silver and gold, made by human hands.
5 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
They have mouths, but cannot speak; they have eyes, but cannot see.
6 zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
They have ears, but cannot hear; they have noses, but cannot smell.
7 Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
They have hands, but cannot feel; they have feet, but cannot walk: no sound comes from their throats.
8 Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
Their makers become like them, so do all who trust in them.
9 Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
O Israel, trust in the Lord: he is their help and their shield.
10 Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
House of Aaron, trust in the Lord: he is their help and their shield.
11 Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
You who fear the Lord, trust in the Lord he is their help and their shield.
12 Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
The Lord, mindful of us, will bless us: he will bless the house of Israel, he will bless the house of Aaron.
13 Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
He will bless those who fear the Lord, the small and the great together.
14 Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
May the Lord add to your numbers to you and to your children.
15 Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
Blessed be you of the Lord, creator of heaven and earth.
16 Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
The heavens are the heavens of the Lord, but the earth has he given to people.
17 Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
The dead cannot praise the Lord, nor those who go down into silence.
18 bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.
But we will bless the Lord from now and for evermore. Hallelujah.

< Zaburi 115 >