< Zaburi 114 >

1 Israeli ilipotoka Misri, na nyumba ya Yakobo toka kutoka katika wale watu wa kigeni,
When Israel went out of Egypt, Jacob’s house from a barbarous people,
2 Yuda ilifanyika kuwa mahali pake patakatifu, Ufalme wa Israeli.
God chose Judah for himself, Israel became his kingdom.
3 Bahari iliona ikakimbia; Yordani ilirudi nyuma.
The sea saw it, and fled, Jordan river ran backwards.
4 Milima iliruka kama kondoo waume, vilima viliruka kama wana-kondoo.
Mountains skipped like rams, hills like the young of the flock.
5 Ewe Bahari kwa nini ulikimbia? Yordani kwa nini ulirudi nyuma?
Why, sea, do you flee? Jordan, why run backwards?
6 Milima, kwa nini uliruka kama kondoo waume? Enyi vilima wadogo, kwa nini mliruka kama wana-kondoo?
Mountains, why skip ram-like? Why, hills, like the young of the flock?
7 Tetemeka, ee nchi, mbele za Bwana, uweponi mwa Mungu wa Yakobo.
Earth, tremble before the Lord, at the presence of Jacob’s God,
8 Aligeuza mwamba kuwa ziwa la maji, jiwe gumu kuwa chemchem.
who turns rocks into pools of water, and flint into fountains of water.

< Zaburi 114 >