< Zaburi 115 >

1 Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
Not to us, O Lord, not to us, but to thy name give glory, because of thy mercy and thy truth;
2 Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
lest at any time the nations should say, Where is their God?
3 Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
But our God has done in heaven and on earth, whatsoever he has pleased.
4 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
The idols of the nations are silver and gold, the works of men's hands.
5 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
They have a mouth, but they cannot speak; they have eyes, but they cannot see:
6 zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
they have ears, but they cannot hear; they have noses, but they cannot smell;
7 Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
they have hands, but they cannot handle; they have feet, but they cannot walk: they cannot speak through their throat.
8 Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
Let those that make them become like to them, and all who trust in them.
9 Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
The house of Israel trusts in the Lord: he is their helper and defender.
10 Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
The house of Aaron trusts in the Lord: he is their helper and defender.
11 Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
They that fear the Lord trust in the Lord: he is their helper and defender.
12 Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
The Lord has remembered us, and blessed us: he has blessed the house of Israel, he has blessed the house of Aaron.
13 Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
He has blessed them that fear the Lord, both small and great.
14 Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
The Lord add [blessings] to you and to your children.
15 Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
Blessed are ye of the Lord, who made the heaven and the earth.
16 Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
The heaven of heavens [belongs] to the Lord: but he has given the earth to the sons of men.
17 Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
The dead shall not praise thee, O Lord, nor any that go down to Hades.
18 bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.
But we, the living, will bless the Lord, from henceforth and for ever.

< Zaburi 115 >