< Zaburi 111 >

1 Msifuni Yahwe. Nitamshukuru Yahwe kwa moyo wangu wote katikati ya kusanyiko la wanye haki, na katika mkutano.
Daré gracias a Yavé con todo [mi] corazón En la compañía de los rectos y en la congregación.
2 Kazi za Yahwe ni kuu, zikisubiriwa na wale wazitamanio.
Grandes son las obras de Yavé, Estudiadas por todos los que se deleitan en ellas.
3 Kazi yake ni adhama na utukufu, na haki yake yadumu milele.
Espléndida y majestuosa es su obra, Y su justicia permanece para siempre.
4 Hufanya mambo makuu ambayo yatakumbukwa; Yahwe ni mwenye huruma na neema.
Hizo memorables sus maravillas. Clemente y misericordioso es Yavé.
5 Huwapa chakula wafuasi wake waaminifu. Siku zote atalikumbuka agano lake.
Dio alimento a los que le temen. Para siempre se acordará de su Pacto.
6 Alionesha uweza wa kazi zake kwa watu wake kwa kuwapa urithi wa mataifa.
El poder de sus obras manifestó a su pueblo Al darle la heredad de las naciones.
7 Kazi za mikono yake ni za kuaminika na haki; maagizo yake yote ni ya kuaminika.
Las obras de sus manos son verdad y justicia. Todos sus Preceptos son firmes.
8 Yamethibitika milele, yamefanywa katika uaminifu na vizuri.
Afirmados eternamente y para siempre, Hechos con verdad y rectitud.
9 Aliwapa ushindi watu wake; aliliteuwa agano lake milele; jina lake ni takatifu na lakutisha.
Envió redención a su pueblo. Estableció su Pacto para siempre. Santo y asombroso es su Nombre.
10 Kumcha Yahwe ni mwanzo wa hekima; wale washikao maagizo yake wana uelewa mzuri. Sifa yake yadumu milele.
El principio de la sabiduría es el temor a Yavé. Buen entendimiento tienen todos los que lo practican. Su alabanza permanece para siempre.

< Zaburi 111 >