< Zaburi 110 >

1 Yahwe humwambia bwana wangu, “Kaa mkono wangu wa kuume mpaka nitakapowaweka adui zako chini ya miguu yako.”
[A Psalm by David.] Jehovah says to my Lord, "Sit at my right hand, until I make your enemies a footstool for your feet."
2 Yahwe atainyosha fimbo ya nguvu yako toka Sayuni; utawale kati ya adui zako.
Jehovah will send forth the rod of your strength out of Zion. Rule in the midst of your enemies.
3 Siku ile ya uweza wako watu wako watakufuata wakiwa katika mavazi matakatifu ya hiari yao wenyewe; tokea tumbo la alfajiri ujana wako utakuwa kwako kama umande.
Your people offer themselves willingly on the day of your power. On the holy mountains at sunrise the dew of your youth will be yours.
4 Yahwe ameapa, na hatabadilika: “Wewe ni kuhani milele, baada ya namna ya Melkizedeki.”
Jehovah has sworn, and will not change his mind: "You are a priest forever in the order of Melchizedek."
5 Bwana yuko mkono wako wa kuume. Siku ile ya hasira yake atawaua wafalme.
Jehovah is at your right hand. He will crush kings in the day of his wrath.
6 Yeye atahukumu matifa; ataujaza uwanja wa vita kwa maiti; atawauwa viongozi kaitka nchi nyingi.
He will judge among the nations. He will heap up dead bodies. He will shatter the head throughout a vast territory.
7 Atakunywa maji ya kijito njiani, kisha baada ya ushindi atainua kichwa chake juu.
He will drink of the brook in the way; therefore he will lift up his head.

< Zaburi 110 >