< Zaburi 11 >

1 Ni kwako Yahweh ninapata usalama; ni kwa namna gani utasema na mimi, “Ruka kama ndege hadi mlimani”?
To the Overseer. — By David. In Jehovah I trusted, how say ye to my soul, 'They moved [to] Thy mountain for the bird?
2 Tazama! Waovu wana andaa pinde zao. Wana tayarisha gizani mishale yao kwenye kamba ili kufyatua mioyo ya wenye haki.
For lo, the wicked tread a bow, They have prepared their arrow on the string, To shoot in darkness at the upright in heart.
3 Ikiwa misingi imeharibiwa, mwenye haki atafanya nini?
When the foundations are destroyed, The righteous — what hath he done?
4 Yahweh yuko katika hekalu takatifu; macho yake yanatazama, yakiuchunguza ubinadamu.
'Jehovah [is] in his holy temple: Jehovah — in the heavens [is] His throne. His eyes see — His eyelids try the sons of men.
5 Yahweh huwachunguza wote wenye haki na waovu, bali huwachukia wapendao kuwaumiza wengine.
Jehovah the righteous doth try. And the wicked and the lover of violence, Hath His soul hated,
6 Yeye huwanyeshea waovu makaa ya mawe na moto wa jehanamu; upepo uunguzao utakuwa ni sehemu yao kutoka katika kikombe chake!
He poureth on the wicked snares, fire, and brimstone, And a horrible wind [is] the portion of their cup.
7 Kwa kuwa Yahweh ni mwenye haki, Naye hupenda haki; wenye haki watauona uso wake.
For righteous [is] Jehovah, Righteousness He hath loved, The upright doth His countenance see!'

< Zaburi 11 >