< Zaburi 109 >

1 Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
Gott meines Lobes, schweig nicht stille!
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
Denn der Mund des Ungerechten und der Mund des Truges haben wider mich sich geöffnet, sie reden mit mir mit Zungen der Lüge.
3 Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
Und mit des Hasses Worten umgeben sie mich, und streiten ohne Ursache wider mich.
4 Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
Für meine Liebe sind sie meine Widersacher; ich aber bin im Gebet.
5 Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
Und sie tun Böses mir, statt Gutes, und Haß für meine Liebe.
6 Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
Bestelle einen Ungerechten über ihn, und lasse Satanas ihm zur Rechten stehen.
7 Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
Wird er gerichtet, gehe er als Ungerechter hervor und zur Sünde werde ihm sein Gebet!
8 Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
Es sollen seiner Tage wenig sein, sein Amt nehme ein anderer.
9 Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
Seine Söhne seien Waisen und sein Weib eine Witwe.
10 Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
Und lasse umherwandern seine Söhne und betteln und nachsuchen aus ihren Verödungen.
11 Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
Es umstricke der Gläubiger alles, was er hat, und Fremde rauben seine Arbeit.
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
Keiner reiche ihm Barmherzigkeit dar, und keiner sei gnädig seinen Waisen!
13 Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
Seine Nachkommen werden ausgerottet! ihr Name im anderen Geschlecht ausgewischt!
14 Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
Es müsse seiner Väter Missetat bei Jehovah gedacht und seiner Mutter Sünde nicht ausgewischt werden.
15 Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
Sie sollen beständig vor Jehovah sein, daß ihr Gedächtnis Er ausrotte von der Erde.
16 Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
Weil Er nicht gedachte Barmherzigkeit zu tun, und den elenden Mann und den Dürftigen verfolgte und den, so verzagten Herzens, daß er ihn töte.
17 Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
Und er liebte den Fluch, so komme der über ihn; und er hatte keine Lust am Segen, so sei er ferne von ihm!
18 Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
Und er ziehe Fluch an, wie sein Obergewand, und er komme in sein Inneres wie Wasser, und wie Öl in seine Gebeine.
19 Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
Er sei ihm wie ein Kleid, das ihn umhüllt, und wie eine Umgürtung, die beständig ihn gürtet.
20 Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
Dies sei die Belohnung meiner Widersacher von Jehovah, und derer, so Böses reden wider meine Seele.
21 Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
Und Du, Jehovah, Herr, handle mit mir um Deines Namens willen; denn gut ist Deine Barmherzigkeit, errette mich.
22 Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
Denn elend bin ich und dürftig, und durchbohrt ist mein Herz in meinem Inneren.
23 Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
Wie der Schatten, wenn er sich neigt, gehe ich dahin, wie die Heuschrecke werde ich abgeschüttelt.
24 Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
Meine Knie straucheln vom Fasten, und mein Fleisch fällt ab vom Fett.
25 Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
Und ich bin ihnen zur Schmach; sie sehen mich und nicken mit dem Kopf.
26 Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
Stehe mir bei, Jehovah, mein Gott, rette mich nach Deiner Barmherzigkeit.
27 Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
Und lasse sie wissen, daß das Deine Hand ist, daß Du, Jehovah, es tust.
28 Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
Fluchen sie, so segne Du, stehen sie auf, so lasse sie beschämt werden! Aber Dein Knecht müsse fröhlich sein!
29 Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
Meine Widersacher müssen mit Schande angezogen werden, und mit ihrer Scham umhüllt werden wie mit einem Oberkleid.
30 Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
Ich will Jehovah sehr danken mit meinem Mund, und in Vieler Mitte will ich Ihn loben.
31 Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.
Denn Er steht dem Dürftigen zur Rechten, ihn zu retten von denen, die seine Seele richten.

< Zaburi 109 >