< Zaburi 109 >

1 Zaburi ya Daudi. Mungu ninaye msifu, usinyamaze kimya.
God of my tehilah ·praise song·, don’t remain silent,
2 Kwa maana waovu na wadanganyifu wananishambulia; wanazungumza uongo dhidi yangu.
for they have opened the mouth of the wicked and the mouth of deceit against me. They have spoken to me with a lying tongue.
3 Wananizunguka na kusema mambo ya chuki, na wananishambulia bila sababu.
They have also surrounded me with words of hatred, and fought against me without a cause.
4 Wananilipa kashfa badala ya upendo, lakini mimi ninawaombea.
Making teshuvah ·complete return· for my love, they are my adversaries; but I am in prayer.
5 Wananilipa uovu badala ya mema, na wanachukia upendo wangu.
They have rewarded me evil for good, and hatred for my love.
6 Teua mtu mwovu aliye adui zaidi kama watu hawa; teua mshitaki asimame mkono wake wa kuume.
Set a wicked man over him. Let an adversary stand at his right hand.
7 Na atakapohukumiwa, aonekane na hatia; maombi yake yachukuliwe kuwa ni dhambi.
When he is judged, let him come out guilty. Let his prayer be turned into sin.
8 Siku zake na ziwe chahe; mamlaka yake na yachukuliwe na mtu mwingine.
Let his days be few. Let another take his office.
9 Watoto wake wawe yatima, na mke wake awe mjane.
Let his children be fatherless, and his wife a widow.
10 Watoto wake wenye kutanga tanga na kuombaomba, wakiondoka katika nyumba zao zilizo haribika na kuomba chakula au pesa kwa wapita njia.
Let his children be wandering beggars. Let them be sought from their ruins.
11 Mdai na achukue vitu vyake vyote amilikivyo; wageni wateke mapato ya kazi yake.
Let the creditor seize all that he has. Let strangers plunder the fruit of his labor.
12 Asiwepo mtu yeyote wa kumfanyia wema; mtu yeyote asiwahurumie yatima wake.
Let there be no one to extend kindness to him, neither let there be anyone to have pity on his orphan children.
13 Watoto wake waangamizwe; majina yao na yafutwe katika kizazi kijacho.
Let his posterity be cut off. In the generation following let their name be blotted out.
14 Uovu wa baba zake utajwe kwa Yahwe; na dhambi ya mama yake isisahaulike.
Let the iniquity of his fathers be remembered by Adonai. Don’t let the sin of his mother be blotted out.
15 Hatia zao na ziwe mbele ya Yahwe siku zote; Yahwe na aiondoe kumbukumbu yao duniani.
Let them be before Adonai continually, that he may cut off their memory from the earth;
16 Yahwe na afanye hivi kwa sababu mtu huyu kamwe hakusumbuka kuonesha uaminifu wa agano wowote, lakini badala yake aliwasumbua wanyonge, wahitaji, na kuwaua walio vunjika moyo.
because he didn’t remember to show kindness, but persecuted the poor and needy man, the broken in heart, to kill them.
17 Alipenda kulaani; na imrudie juu yake. Alichukia kubariki; baraka zozote na zisije kwake.
Yes, he 'ahav ·affectionately loved· cursing, and it came to him. He didn’t delight in blessing, and it was far from him.
18 Alijivika kulaani kana kwamba ni vazi lake, na laana yake iliingia ndani yake kama maji, na kama mafuta mifupani mwake.
He clothed himself also with cursing as with his garment. It came into his inward parts like water, like oil into his bones.
19 Laana zake na ziwe kwake kama vazi avaalo kujifunika mwenyewe, na kama mkanda avaao kila siku.
Let it be to him as the clothing with which he covers himself, for the belt that is always around him.
20 Na haya yawe malipo ya mshitaki wangu kutoka kwa Yahwe, ya wale wasemao mambo maovu juu yangu.
This is the reward of my adversaries from Adonai, of those who speak evil against my soul.
21 Yahwe Bwana wangu, unishughulikie kwa wema kwa ajili ya jina lako. Kwa sababu uaminifu wa agano lako ni mwema, uniokoe.
But deal with me, Adonai the Lord, for your name’s sake, because your cheshed ·loving-kindness· is good, deliver me;
22 Kwa maana ni mnyonge na muhitaji, na moyo wangu umejeruhiwa ndani yangu.
for I am poor and needy. My heart is wounded within me.
23 Ninatoweka kama kivuli cha jioni; ninapeperushwa kama nzige.
I fade away like an evening shadow. I am shaken off like a locust.
24 Magoti yangu ni dhaifu kutokana na kufunga; ninakuwa mwembamba na mifupa.
My knees are weak through fasting. My body is thin and lacks fat.
25 Nimedharauliwa na washitaki wangu; wanionapo; hutikisa vichwa vyao.
I have also become a reproach to them. When they see me, they shake their head.
26 Nisaidie, Yahwe Mungu wangu; uniokoe kwa uaminifu wa agano lako.
Help me, Adonai, my God. Save me according to your cheshed ·loving-kindness·;
27 Nao wajue kuwa wewe umefanya haya, kwamba wewe, Yahwe, umetenda haya.
that they may know that this is your hand; that you, Adonai, have done it.
28 Ingawa wananilaani, tafadhali unibariki; wanishambuliapo, waaibishwe, lakini mtumishi wako afurahi.
They may curse, but you bless. When they arise, they will be shamed, but your servant shall rejoice.
29 Washitaki wangu na wavishwe kwa aibu; wavae aibu yao kama vazi.
Let my adversaries be clothed with dishonor. Let them cover themselves with their own shame as with a robe.
30 Kwa kinywa changu ninatoa shukrani kuu kwa Yahwe; nitamsifu yeye katikati ya kusanyiko.
I will give great thanks to Adonai with my mouth. Yes, I will yadah ·extend hands in thankful praise· to him among the multitude.
31 Maana nitasimama mkono wa kuume wa mhitaji, ili nimuokoe dhidi ya wale wanao muhukumu.
For he will stand at the right hand of the needy, to save him from those who judge his soul.

< Zaburi 109 >