< Zaburi 108 >

1 Ee Mungu, moyo wangu u thabiti; nitaimba, naam, nitaimba sifa pia kwa moyo mkuu.
My heart is steadfast, God. I will sing zahmar ·musical praise· and I will give kavod ·weighty glory·.
2 Amka, kinanda na kinubi; nitaamka alfajiri.
Wake up, harp and lyre! I will wake up the dawn.
3 Nitakushukuru wewe, Yahwe, kati ya watu; nitakuimbia sifa kati ya mataifa.
I will yadah ·extend hands in thankful praise· to you, Adonai, among the nations. I will sing zahmar ·musical praise· to you among the peoples.
4 Kwa maana uaminifu wa agano lako ni mkuu juu ya mbingu; na uaminifu wako wafika mawinguni.
For your cheshed ·loving-kindness· is great above the heavens. Your faithfulness reaches to the skies.
5 Ee Mungu, uinuliwe, juu ya mbingu, na utukufu wako utukuke juu ya nchi.
Be exalted, God, above the heavens! Let your kavod ·weighty glory· be over all the earth.
6 Ili kwamba wale uwapendao waokolewe, utuokoe sisi kwa mkono wako wa kuume na unijibu.
That your yadid ·beloved· may be delivered, save with your right hand, and answer us.
7 Mungu ameongea katika utakatifu wake; “Nitashangilia; nitaigawanya Shekemu na nitalipima bonde la Sukothi.
God has spoken from his sanctuary: “In triumph, I will divide Shechem, and measure out the valley of Sukkot.
8 Gileadi ni yangu, na manase ni yangu; Ephraimu ni nguvu ya kichwa changu; Yuda ni fimbo yangu ya kifalme.
Gilead is mine. Manasseh [Causing to forget] is mine. Ephraim [Fruit] also is my helmet. Judah [Praised] is my scepter.
9 Moabu ni bakuli langu la kunawia; nitatupa kiatu changu juu ya Edomu; nitapaza sauti katika ushindi kwa ajili ya Filisti.
Moab [From father] is my wash pot. I will toss my sandal on Edom [Red]. I will shout over Philistia.”
10 Ni nani atakaye nipeleka kwenye mji imara? Ni nani atakayeniongoza mpaka Edomu?”
Who will bring me into the fortified city? Who has led me to Edom [Red]?
11 Ee Mungu, sio wewe uliyetukataa? Hauendi vitani na jeshi letu.
Haven’t you rejected us, God? You don’t go out, God, with our armies.
12 Utupe msaada dhidi ya adui yetu, maana msaada wa wanadamu ni bure.
Give us help against the enemy, for the help of man is vain.
13 Tutashinda kwa msaada wa Mungu; atawakanyaga kwa adui zetu.
Through God, we will do valiantly. For it is he who will tread down our enemies.

< Zaburi 108 >