< Zaburi 107 >

1 Mshukuruni Yahwe, maana ni mwema, na uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Alleluia. Give thanks to the Lord, for he is good; for his mercy [endures] for ever.
2 Waseme hivi waliokombolewa na Yahwe, wale aliowaokoa toka mkononi mwa adui.
Let them say [so] who have been redeemed by the Lord, whom he has redeemed from the hand of the enemy;
3 Yeye amewakusanya kutoka nchi za kigeni, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
and gathered them out of the countries, from the east, and west, and north, and south.
4 Walitanga-tanga janwani katika njia ya nyika hawakuona mji wa kuishi.
They wandered in the wilderness in a dry land; they found no way to a city of habitation.
5 Kwa sababu walikuwa na njaa na kiu, walikata tamaa kutokana na uchovu.
Hungry and thirsty, their soul fainted in them.
6 Kisha walimuita Yahwe katika shida yao, naye aliwaokoa toka katika dhiki yao.
Then they cried to the Lord in their affliction, and he delivered them out of their distresses.
7 Aliwaongoza kupitia njia ya moja kwa moja waweze kwenda mjini kuishi humo.
And he guided them into a straight path, that they might go to a city of habitation.
8 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliowatendea wanadamu!
Let them acknowledge to the Lord his mercies, and his wonderful works to the children of men.
9 Maana hutosheleza shauku za walio na kiu, na hamu ya wale wenye njaa yeye huwashibisha kwa mambo mema.
For he satisfies the empty soul, and fills the hungry [soul] with good things,
10 Baadhi walikaa katika giza na uvuli wa mauti, walifungwa katika mateso na minyororo.
[even] them that sit in darkness and the shadow of death, fettered in poverty and iron;
11 Hii ni kwa sababu walikuwa wameliasi neno la Mungu na walikataa maelekezo ya Aliye Juu.
because they rebelled against the words of God, and provoked the counsel of the Most High.
12 Aliinyenyekesha mioyo yao kupitia magumu; walipata mashaka na hakukuwa na mmoja wa kuwasaidia.
So their heart was brought low with troubles; they were weak, and there was no helper.
13 Kisha wakamwita Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Then they cried to the Lord in their affliction, and he saved them out of their distresses.
14 Aliwatoa gizani na kwenye uvuli wa mauti na kuvunja vifungo vyao.
And he brought them out of darkness and the shadow of death, and broke their bonds asunder.
15 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
Let them acknowledge to the Lord his mercies, and his wonders to the children of men.
16 Kwa maana amevunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
For he broke to pieces the brazen gates, and crushed the iron bars.
17 Walikuwa wapumbavu katika njia zao za uasi na kuteswa kwa sababu ya dhambi zao.
He helped them out of the way of their iniquity; for they were brought low because of their iniquities.
18 Walipoteza hamu yao ya kula chakula chochote, na waliyakaribia malango ya kifo.
Their soul abhorred all meat; and they drew near to the gates of death.
19 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Then they cried to the Lord in their affliction, and he saved them out of their distresses.
20 Alituma neno lake na likawaponya, na akawaokoa kutoka katika uharibifu wao.
He sent his word, and healed them, and delivered them out of their destructions.
21 Oh ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyoyatenda kwa wanadamu!
Let them acknowledge to the Lord his mercies, and his wonderful works to the children of men.
22 Na watoe dhabihu ya shukrani na kutangaza matendo yake kwa kuimba.
And let them offer to him the sacrifice of praise, and proclaim this works with exultation.
23 Baadhi husafiri baharini katika meli na kufanya biashara juu ya bahari.
They that go down to the sea in ships, doing business in many waters;
24 Hawa huona matendo ya Yahwe na maajabu yake baharini.
these [men] have seen the works of the Lord, and his wonders in the deep.
25 Kwa maana aliamuru na alivumisha upepo wa dhoruba ambao uliyainua juu mawimbi ya baharini.
He speaks, and the stormy wind arises, and its waves are lifted up.
26 Walipanda juu mawinguni na kushuka vilindini. Nafsi zao ziliyeyuka katika dhiki.
They go up to the heavens, and go down to the depths; their soul melts because of troubles.
27 Waliyumba-yumba na kupepesuka kama walevi na hawakujua la kufanya.
They are troubled, they stagger as a drunkard, and all their wisdom is swallowed up.
28 Kisha walimlilia Yahwe katika shida yao, naye akawatoa katika dhiki yao.
Then they cry to the Lord in their affliction, and he brings them out of their distresses.
29 Aliituliza dhoruba, na mawimbi yakatulia.
And he commands the storm, and it is calmed into a gentle breeze, and its waves are still.
30 Ndipo walifurahia kwa sababu bahari ilikuwa shwali, na aliwaleta kwenye bandari waliyoitamani.
And they are glad, because they are quiet; and he guides them to their desire haven.
31 Oh, ili watu wamsifu Yahwe kwa ajili ya uaminifu wa agano lake na kwa mambo ya ajabu aliyowatendea wanadamu!
Let them acknowledge to the Lord his mercies, and his wonderful works to the children of men.
32 Wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu na wamsifu yeye katika baraza la viongozi.
Let them exalt him in the congregation of the people, and praise him in the seat of the elders.
33 Aligeuza mito ikwa jangwa, chemchem ya maji ikawa nchi kame,
He turns rivers into a desert, and streams of water into a dry land;
34 na nchi ya matunda mengi ikawa nchi isiyozaa kwa sababu ya uovu wa watu wake.
a fruitful land into saltness, for the wickedness of them that dwell in it.
35 Aligeuza jangwa likawa ziwa la maji na nchi kame ikawa chemchem ya maji.
He turns a wilderness into pools of water, and a dry land into streams of water.
36 Aliwakalisha huko wenye njaa, nao walijenga mji na kuishi humo.
And there he causes the hungry to dwell, and they establish for themselves cities of habitation.
37 Walijenga mji ili kupanda mimea shambani, kupanda mizabibu, na kuleta humo mazao tele.
And they sow fields, and plant vineyards, and they yield fruit of increase.
38 Yeye huwabariki wameongezeka sana katika hesabu. Haachi mifugo yao ipungue katika hesabu.
And he blesses them, and they multiply exceedingly, and he diminishes not the number of their cattle.
39 Kisha wakapungua na kudhilika kwa dhiki na mateso.
Again they become few, and are brought low, by the pressure of evils and pain.
40 Akawamwagia viongozi dharau na akawafanya wazunguke katika jangwa, mahali pasipo na njia.
Contempt is poured upon their princes, and he causes them to wander in a desert and trackless land.
41 Lakini aliwalinda wahitaji dhidi ya mateso na kujali kwa ajili ya familia yake kama kundi la kondoo.
But he helps the poor out of poverty, and makes [him] families as a flock.
42 Wenye haki wataona hili na kufurahi, na uovu wote utaona na kufunga kinya chake.
The upright shall see and rejoice; and all iniquity shall stop her mouth.
43 Yeyote mwenye hekima anapaswa kuyaangalia haya na kutafakari juu ya matendo ya uaminifu wa agano la Yahwe.
Who is wise, and will observe these things, and understand the mercies of the Lord?

< Zaburi 107 >