< Zaburi 106 >

1 Msifuni Yahwe. Mshukuruni Yahwe, kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Alleluia. Give thanks to the Lord; for he is good: for his mercy [endures] for ever.
2 Ni nani awezaye kuyahesabu mataendo makuu ya yahwe au kutangaza katika ukamilifu sifa zote za matendo yake ya kuaminika.
Who shall tell the mighty acts of the Lord? [who] shall cause all his praises to be heard?
3 Wamebarikiwa wale watendao yaliyo mema na matendo yao yaliyo haki siku zote.
Blessed are they that keep judgement, and do righteousness at all times.
4 Ukumbuke, Ee Yahwe, unapowaonesha watu wako neema; unisaidie unapowaokoa.
Remember us, O Lord, with the favour [you have] to your people: visit us with your salvation;
5 Ndipo nitaona mafanikio ya wateule wako, wakifurahia katika furaha ya taifa lako, na utukufu pamoja na urithi wako.
that we may behold the good of your elect, that we may rejoice in the gladness of your nation, that we may glory with your inheritance.
6 Tumefanya dhambi kama babu zetu, tumekosea, na kufanya uovu.
We have sinned with our fathers, we have transgressed, we have done unrighteously.
7 Baba zetu hawakuyatambua matendo yako ya ajabu katika Misri; walipuuzia matendo yako mengi ya uaminifu wa agano; waliasi penye bahari, bahari ya Shamu.
Our fathers in Egypt understood not your wonders, and remembered not the multitude of your mercy; but provoked [him] as they went up by the Red Sea.
8 Hata hivyo, yeye aliwaokoa kwa ajili ya jina lake ili kwamba aweze kuzifunua nguvu zake.
Yet he saved them for his name's sake, that he might cause his mighty power to be known.
9 Aliikemea Bahari ya Shamu, nayo ikakauka. Kisha akawaongoza vilindini, kana kwamba ni jangwani.
And he rebuked the Red Sea, and it was dried up: so he led them through the deep as through the wilderness.
10 Aliwaokoa kutoka mkononi mwa wale waliowachukia, na aliwaokoa kutoka mkononi mwa adui.
And he saved them out of the hand of them that hated [them], and redeemed them out of the hand of the enemy.
11 Lakini maji yaliwafunika washindani wao; hakuna hata mmoja aliye okolewa.
The water covered those that oppressed them: there was not one of them left.
12 Ndipo waliyaamini maneno yake, nao waliimba sifa zake.
Then they believed his words, and celebrated his praise.
13 Lakini walisahau haraka kile alichofanya; hawakuyasubiri maelekezo yake.
They made haste, they forgot his works; they waited not for his counsel.
14 Walikuwa na tamaa isiyotoshelezwa jangwani, wakamjaribu Mungu nyikani.
And they lusted exceedingly in the wilderness, and tempted God in the dry [land].
15 Aliwapa ombi lao, lakini alituma gonjwa ambalo lilishambulia miili yao.
And he gave them their request, and sent fullness into their souls.
16 Katika kambi wakawa na wivu juu Musa na Haruni, kuhani mtakatifu wa Yahwe.
They provoked Moses also in the camp, and Aaron the holy one of the Lord.
17 Nchi ilifunguka na ilimmeza Dathani na iliwafunika wafuasi wa Abiramu.
The earth opened and swallowed up Dathan, and closed upon the congregation of Abiron.
18 Moto uliwaka kati yao; moto uliwaangamiza waovu.
And a fire was kindled in their congregation, and a flame burnt up the sinners.
19 Walitengeneza ndama huko Horebu na kuabudu sanamu ya kuyeyuka.
And they made a calf in Choreb, and worshipped the graven image,
20 Wakaubadili utukufu wa Mungu kuwa mfano wa ng'ombe alaye majani.
and they changed their glory into the similitude of a calf that feeds on grass.
21 Walimsahau Mungu wokozi wao, aliyefanya mambo makuu katika Misri.
They forgot God that saved them, who had wrought great deeds in Egypt;
22 Alifanya matendo ya ajabu katika nchi ya Hamu na matendo makuu penye Bahari ya Shamu.
wondrous [works] in the land of Cham, and terrible things at the Red Sea.
23 Mungu angetangaza uharibifu wao, kama sio Musa, mteule wake, aliingilia kati kugeuza hasira yake dhidi ya kuwaangamiza.
So he said that he would have destroyed them, had not Moses his chosen stood before him in the breach, to turn [him] away from the fierceness of his anger, so that he should not destroy them.
24 Kisha waliidharau nchi yenye matunda; hawakuiamini ahadi yake,
Moreover they set at nothing the desirable land, and believed not his word.
25 bali walilalamiaka katika mahema yao, na hawakumtii Yahwe.
And they murmured in their tents: they listened not to the voice of the Lord.
26 Kwa hiyo aliinua mkono wake na kuapa kwao kuwa atawaacha wafe jangwani,
So he lifted up his hand against them, to cast them down in the wilderness;
27 akitawanya uzao wao kati ya mataifa, na kuwatawanya katika nchi za kigeni.
and to cast down their seed amongst the nations, and to scatter them in the countries.
28 Waliabudu Baal ya Poeri na walizila dhabihu zilizotolewa kwa wafu.
They were joined also to Beelphegor, and ate the sacrifices of the dead. And they provoked him with their devices;
29 Walimkasirisha kwa matendo yao, na pigo la gonjwa baya liliwashambulia kati yao.
and destruction, was multiplied amongst them.
30 Ndipo Finehasi aliinuka kuingilia kati, na pigo likakoma.
Then Phinees stood up, and made atonement: and the plague ceased.
31 Ilihesabika kwake kama tendo la haki kwa vizazi vyote hata milele.
And it was counted to him for righteousness, to all generations for ever.
32 Pia walimkasirisha Yahwe penye maji ya Meriba, na Musa aliteseka kwa ajili yao.
They provoked him also at the water of Strife, and Moses was hurt for their sakes;
33 Walimghadhabisha Musa naye akaongea haraka.
for they provoked his spirit, and he spoke [unadvisedly] with his lips.
34 Hawakuyaharibu mataifa kama Yahwe alivyowaamuru,
They destroyed not the nations which the Lord told them [to destroy];
35 bali walichangamana na mataifa na walijifunza njia zao
but were mingled with the heathen, and learnt their works.
36 nao waliabudu sanamu, nazo zikawa mtego kwao.
And they served their graven images; and it became an offence to them.
37 Waliwatoa wana wao na binti zao kwa mapepo.
And they sacrificed their sons and their daughters to devils,
38 Walimwaga damu isiyo na hatia, damu ya wana na binti zao, ambao waliwatoa kama dhabihu kwa sanamu za Kanaani, waliinajisi nchi kwa damu.
and shed innocent blood, the blood of their sons and daughters, whom they sacrificed to the idols of Chanaan; and the land was defiled with blood.
39 Walinajisiwa kwa matendo yao; katika matendo yao walikuwa kama malaya.
and was polluted with their works; and they went a whoring with their own devices.
40 Hivyo Yahwe aliwakasilikia watu wake, akawadharau watu wake mwenyewe.
So the Lord was very angry with his people, and he abhorred his inheritance.
41 Akawaruhusu mataifa, na wale walio wachukia wakawatawala.
And he delivered them into the hands of [their] enemies; and they that hated them ruled over them.
42 Maadui zao wakawaonea, wakatiishwa chini ya mamlaka yao.
Ands their enemies oppressed them, and they were brought down under their hands.
43 Mara nyingi alienda kuwasaidia, lakini waliendelea kuasi nao walishushwa chini kwa dhambi zao wenyewe.
Many a time he delivered them; but they provoked him by their counsel, and they were brought low by their iniquities.
44 Hata hivyo, aliiangalia dhiki yao aliposikia kilio chao kwa ajili ya msaada.
You the Lord looked upon their affliction, when he heard their petition.
45 Alikumbuka agano lake pamoja nao na alijirudi kwa sababu ya upendo wake thabiti.
And he remembered his covenant, and repented according to the multitude of his mercy.
46 Aliwafanya wote waliowateka wawahurumie.
And he caused them to be pitied in the sight of all who carried them captive.
47 Utuokoe, Ee Yahwe, Mungu wetu. Utukusanye kutoka kati ya mataifa ili kwamba tuweze kulishukuru jina lako takatifu na utukufu katika sifa zako. Yahwe,
Save us, O Lord our God, and gather us from amongst the heathen, that we may give thanks to your holy name, that we may glory in your praise.
48 Mungu wa Israeli, na asifiwe toka milele na milele. watu wote walisema, “Amen.” Msifuni Yahwe. Kitabu cha tano.
Blessed be the Lord God of Israel from everlasting and to everlasting; and all the people shall say, Amen, Amen.

< Zaburi 106 >