< Zaburi 1 >

1 Amebarikiwa mtu yule asiye enenda katika ushauri wa waovu, au kusimama katika njia ya wenye dhambi, au kukaa katika kusanyiko la wenye mizaha.
Blessed is the man that walketh not in the counsel of the ungodly, nor standeth in the way of sinners, nor sitteth in the seat of scoffers.
2 Bali yeye huifurahia sheria ya Yahwe, na huitafakari sheria yake mchana na usiku.
But his delight is in the law of the LORD; and in his law doth he meditate day and night.
3 Atakuwa kama mti uliopandwa karibu na mkondo wa maji ambao huzaa matunda yake kwa majira yake, ambao majani yake hayakauki; lolote afanyalo litafanikiwa.
And he shall be like a tree planted by the rivers of water, that bringeth forth its fruit in its season; its leaf also shall not wither; and whatever he doeth shall prosper.
4 Waovu hawako hivyo, wao badala yake ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
The ungodly are not so: but are like the chaff which the wind driveth away.
5 Kwa hivyo waovu hawatasimama katika hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
Therefore the ungodly shall not stand in the judgment, nor sinners in the congregation of the righteous.
6 Kwa kuwa Yahweh huikubali njia ya wenye haki, njia ya waovu itaangamizwa.
For the LORD knoweth the way of the righteous: but the way of the ungodly shall perish.

< Zaburi 1 >