< Zaburi 1 >

1 Amebarikiwa mtu yule asiye enenda katika ushauri wa waovu, au kusimama katika njia ya wenye dhambi, au kukaa katika kusanyiko la wenye mizaha.
Blessed is the man who does not walk in the counsel of the wicked, nor stand on the path of sinners, nor sit in the seat of scoffers;
2 Bali yeye huifurahia sheria ya Yahwe, na huitafakari sheria yake mchana na usiku.
but his delight is in Adonai’s Torah ·Teaching·. On his torot ·teachings· he meditates day and night.
3 Atakuwa kama mti uliopandwa karibu na mkondo wa maji ambao huzaa matunda yake kwa majira yake, ambao majani yake hayakauki; lolote afanyalo litafanikiwa.
He will be like a tree planted by the streams of water, that produces its fruit in its season, whose leaf also does not wither. Whatever he does shall prosper.
4 Waovu hawako hivyo, wao badala yake ni kama makapi yapeperushwayo na upepo.
The wicked are not so, but are like the chaff which the wind drives away.
5 Kwa hivyo waovu hawatasimama katika hukumu, wala wenye dhambi katika kusanyiko la wenye haki.
Therefore the wicked shall not stand in the judgment, nor sinners in the congregation of the upright.
6 Kwa kuwa Yahweh huikubali njia ya wenye haki, njia ya waovu itaangamizwa.
For Adonai knows the way of the upright, but the way of the wicked shall perish.

< Zaburi 1 >