< Mithali 8 >

1 Je hekima haiti? Je ufahamu hapazi sauti yake?
He aquí que la sabiduría levanta la voz, y se hace oír la inteligencia.
2 Juu ya kilima kando ya barabara, kwenye njia panda, hekima anasimama.
En las altas cimas, junto a la carretera, en las encrucijadas de los caminos es donde se para.
3 Kando ya njia ya kuingilia mjini, karibu na milango ya mji, anaita kwa sauti.
En las puertas, en las entradas de la ciudad, en los umbrales de las casas, hace ella oír su voz:
4 Watu, ninawaita ninyi na ninapaza sauti yangu kwa wana wa wanadamu.
“A vosotros, mortales, me dirijo, mi voz va a los hijos de los hombres.
5 Ninyi wajinga, jifunzeni hekima, na ninyi mnaochukia maarifa, lazima mjipatieni moyo wa ufahamu.
Aprended, oh necios, la sabiduría, y vosotros, oh insensatos, la inteligencia.
6 Sikiliza na mimi nitasema mambo mazuri na nifumbuapo midomo yangu nitaongea haki.
Escuchadme que voy a deciros cosas magníficas, y mis labios se abrirán para (enseñar) lo recto.
7 Maana kinywa changu hunena uaminifu na midomo yangu huchukia uovu.
Porque verdad proclama mi boca, y mis labios abominan la maldad.
8 Maneno ya kinywa changu yote ni haki; hakuna kilichogeuzwa wala kupotoshwa.
Justos son todos los dichos de mi boca; nada hay en ellos de torcido o perverso.
9 Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
Todos son rectos para quien tiene inteligencia, y justos para quien llegó a entender.
10 Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
Recibid mi instrucción, y no la plata, y la sabiduría, antes que el oro escogido.
11 Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
Pues la sabiduría vale más que perlas, y todas las cosas deseables no la igualan.
12 Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.
Yo, la sabiduría, habito con la prudencia, y poseo el conocimiento más profundo.
13 Hofu ya Mungu ni kuchukia uovu- nachukia majivuno na kiburi, njia ya uovu, na kauli iliyopotoka- hivyo ninavichukia.
Temer a Yahvé es detestar el mal; yo abomino la soberbia, la altivez, el mal camino y la boca perversa.
14 Ninaushauri mzuri na hekima sahihi; mimi ni busara; nguvu zipo kwangu.
Mío es el consejo y la prudencia, mía la inteligencia y mía la fuerza.
15 Kwa njia yangu wafalme hutawala- pia na waungwana, na wote ambao hutawala kwa haki.
Por mí reinan los reyes y los príncipes administran la justicia.
16 Kwa njia yangu wafalme hutawala na waungwana na wote wanaotawala kwa haki.
Por mí mandan los gobernantes, los grandes y todos los jueces de la tierra.
17 Nawapenda wale wanaonipenda, na wale wanaonitafuta kwa bidii, wataniona.
Yo amo a los que me aman; y los que me buscan me hallarán.
18 Kwangu kunautajiri na heshima, utajiri wa kudumu na haki.
En mi mano están la riqueza y la gloria, los bienes duraderos y la justicia.
19 Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, bora hata kuliko dhahabu safi.
Mi fruto es mejor que el oro más puro, y mis productos son mejores que la plata escogida.
20 Ninazalisha kilicho bora kuliko fedha safi. Natembea katika njia ya haki,
Yo voy por las sendas de la justicia por medio del recto camino,
21 katika mapito ambayo huelekea kwenye haki, ili niwape urithi wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.
para dar bienes a mis amigos, y henchir sus tesoros.
22 Yehova aliniumba tokea mwanzo- mwazoni mwa matendo yake ya nyakati za kale.
El Señor me poseyó al principio de sus caminos, antes de sus obras más antiguas.
23 Tokea enzi za kale niliwekwa katika nafasi- tokea kwanza, tokea mwanzo wa dunia.
Desde la eternidad fui constituida, desde los orígenes, antes que existiera la tierra.
24 Kabla ya bahari, mimi nilizaliwa- kabla ya kuwepo chemchemi zenye maji tele.
Antes que los abismos fui engendrada yo; no había aún fuentes ricas en aguas.
25 Kabla ya milima na vilima kuwekwa, mimi nilizaliwa.
Antes que fuesen asentados los montes; antes que los collados fui yo dada a luz,
26 Nilizaliwa kabla ya Yehova hajaiumba dunia wala makonde, hata mavumbi ya kwanza katika dunia.
cuando aún no había creado Él la tierra ni los campos, ni el primer polvo del orbe.
27 Nilikuwepo alipoziimarisha mbingu, wakati alipochora mstari katika sura ya kilindi.
Cuando estableció los cielos, allí estaba yo; cuando trazó el horizonte sobre la faz del abismo;
28 Nilikuwepo alipoimarisha anga la juu na wakati wa kutengeneza kina cha chemchemi.
cuando fijó las nubes en lo alto, y dio fuerza a las aguas de la profundidad;
29 Nilikuwepo alipotengeneza mipaka ya bahari, ili maji yasisambae kuvuka pale alipoyaamuru, na wakati anaamuru misingi ya dunia sehemu ya kukaa.
cuando señaló sus límites al mar, para que las aguas no traspasasen sus orillas; cuando puso los cimientos de la tierra,
30 Nilikuwa kando yake, kama fundistadi mkuu, na mimi nilikuwa furaha yake siku kwa siku, nikifurahi mbele zake daima.
entonces estaba yo con Él, como arquitecto, deleitándome todos los días y me regocijaba delante de Él continuamente.
31 Nilikuwa nikifurahi katika dunia yake yote na furaha yangu ilikuwa kwa wana wa wanadamu.
Me holgaba en el orbe de la tierra, teniendo mi delicia en los hijos de los hombres.
32 Na sasa, wanangu, nisikilizeni, maana wale wazishikao njia zangu watakuwa na furaha.
Y ahora, hijos, oídme: Dichosos aquellos que siguen mis caminos.
33 Sikilizeni fundisho langu na mpate hekima; wala msilipuuze.
Escuchad la instrucción, y sed sabios; y no la rechacéis.
34 Anisikilizaye atakuwa na furaha- kila siku akitazama katika malango yangu, akinisubiri pembeni mwa milango ya masikani yangu.
Bienaventurado el hombre que me oye, y vela a mis puertas día tras día, aguardando en el umbral de mi entrada.
35 Maana yeyote anionaye mimi, anapata uzima, naye atapata kibali kwa Yehova.
Porque quien me halla a mí, ha hallado la vida, y alcanza el favor de Yahvé.
36 Na yeyote asiyeniona mimi, hujiumiza mwenyewe, wote wanaonichukia hupenda mauti.
El que a mí me ofende daña a su propia alma; todos los que me odian, aman la muerte.

< Mithali 8 >