< Mithali 6 >

1 Mwanangu, kama utaweka pesa zako kuwa dhamana kwa mkopo wa jirani yako; kama ukitoa ahadi yako katika mkopo wa mtu usiyemjua,
Hijo mío, si saliste fiador de tu prójimo. Si tendiste tu mano a un extraño,
2 basi umejiwekea mtego mwenyewe na umenaswa kwa maneno ya kinywa chako.
si te ligaste con la palabra de tu boca, y quedaste preso por lo que dijeron tus labios,
3 Mwanagu, ukinaswa kwa maneno yako mwenyewe, fanya haya ili kujiokoa, kwa kuwa umeangukia kwenye mikono ya jirani yako; nenda unyenyekee na ufanye shauri mbele ya jirani yako.
haz esto, hijo mío: Recobra la libertad; ya que has caído en manos de tu prójimo. Ve sin tardanza e importuna a tu amigo.
4 Usiruhusu usingizi katika macho yako wala kope za macho yako kusinzia.
No concedas sueño a tus ojos, ni reposo a tus párpados.
5 Jiokoe mwenyewe kama swala kutoka katika mkono wa mwindaji, kama ndege kutoka katika mkono wa mwinda ndege.
Líbrate, como el corzo, de su mano, como el pájaro de la mano del cazador.
6 Wewe mtu mvivu, mwangalie mchwa, zitafakari njia zake ili kupata busara.
Ve, oh perezoso, a la hormiga; observa su obra y hazte sabio.
7 Hana akida, afisa au mtawala,
No tiene juez, ni superior, ni señor,
8 lakini huandaa chakula chake wakati wa joto na wakati wa mavuno huweka hazina ili kula baadaye.
y se prepara en el verano su alimento, y recoge su comida al tiempo de la mies.
9 Ewe mtu mvivu, utalala hata lini? Wakati gani utainuka usingizini?”
¿Hasta cuándo, perezoso, quedarás acostado? ¿Cuándo despertarás de tu sueño?
10 Lala kidogo, sizia kidogo, kunja mikono kupumzika kidogo” -
Un poco dormir, un poco dormitar, cruzar un poco las manos para descansar;
11 ndipo umasikini wako utakapokujia kama mporaji na uhitaji wako kama askari wa vita.
y te sobrevendrá cual salteador la miseria, y la necesidad cual hombre armado.
12 Mtu asiyefaa-mtu mwovu- huishi kwa kauli za udanganyifu wake,
Hijo de Belial es el hombre inicuo, anda con perversidad en la boca,
13 akipepesa macho yake, akiashilia kwa miguu yake na kusonta kwa videle vyake.
guiña los ojos, hace señas con los pies, habla con los dedos.
14 Hufanya njama za uovu kwa hila ya moyo wake; daima huchochea faraka.
En su corazón habita la perversidad; urde el mal en todo tiempo, y siembra discordias.
15 Kwa hiyo msiba wake utamkumba kwa ghafula, punde atavunjika vibaya wala hatapona.
Por eso vendrá de improviso su ruina, de repente será quebrantado sin que tenga remedio.
16 Kuna vitu sita ambavyo Yehova huvichukia, saba ambavyo ni chukizo kwake.
Seis son las cosas que aborrece Yahvé, y una séptima abomina su alma:
17 Macho ya mtu mwenye kiburi, ulimi wa uongo, mikono inayomwaga damu ya watu maasumu,
Ojos altivos, lengua mentirosa, manos que vierten sangre inocente,
18 moyo unaobuni njama mbaya, miguu inayokimbilia maovu upesi,
corazón que maquina designios perversos, pies que corren ligeros tras el mal,
19 shahidi asemaye uongo na apandaye faraka kati ya ndugu.
testigo falso que respira calumnias, y quien siembra discordia entre hermanos.
20 Mwanangu, itii amri ya baba yako na wala usiyaache mafundisho ya mama yako.
Guarda, hijo mío, la doctrina de tu padre; y no desprecies la enseñanza de tu madre.
21 Uyafunge katika moyo wako siku zote; yafunge kwenye shingo yako.
Tenlas siempre atadas a tu corazón, enguirnalda con ellas tu cuello.
22 utembeapo, yatakuongoza; ulalapo yatakulinda, na uamkapo yatakufundisha.
Te guiarán en tu camino, velarán por ti cuando durmieres; y hablarán contigo al despertar.
23 Maana amri ni taa, na mafundisho ni nuru; kinga za kuadilisha za njia ya uzima.
Porque el precepto es una antorcha, y la ley una luz, y senda de vida son las amonestaciones dadas para corrección.
24 Yanakulinda dhidi ya mwanamke malaya, dhidi ya maneno laini ya uzinzi.
Pues te guardarán de la mala mujer, de los halagos seductores de la ajena.
25 Moyoni mwako usiutamani uzuri wake wala usitekwe katika kope zake.
No codicies en tu corazón la hermosura de ella, no te seduzcan sus ojos.
26 Kulala na malaya inaweza kugharimu bei ya kipande cha mkate, lakini mke wa mtu mwingine inagharimu uzima wako wote.
Pues por la prostituta uno es reducido a un pedazo de pan, mientras la casada va a la caza de una vida preciosa.
27 Je mtu anaweza kubeba moto katika kifua chake bila kuuguza mavazi yake?
¿Acaso puede un hombre llevar fuego en el seno, sin que ardan sus vestidos?
28 Je mtu anaweza kutembea juu ya makaa bila kuchomwa miguu yake?
¿O andar sobre brasas, sin quemarse los pies?
29 Ndivyo alivyo mtu alalaye na mke wa jirani yake; yule alalaye na huyo mke hatakosa adhabu.
Así (sucede con) aquel que se llega a la mujer de su prójimo; no quedará sin castigo quien la tocare.
30 Watu hawawezi kumdharau mwizi kama anaiba ili kukidhi hitaji lake la njaa.
¿No es acaso despreciado el ladrón que roba para saciar su apetito cuando tiene hambre?
31 Walakini akimatwa, atalipa mara saba ya kile alichoiba; lazima atoe kila kitu cha thamani katika nyumba yake.
Si es hallado, ha de pagar siete veces otro tanto, tendrá que dar hasta toda la sustancia de su casa.
32 Mtu anayefanya uzinzi hana akili; hufanya hiyo kwa uharibifu wake mwenyewe.
Quien comete adulterio con una mujer es un insensato; quien hace tal cosa se arruina a sí mismo.
33 Anasitahili aibu na majeraha na fedheha yake haiwezi kuondolewa.
Cosechará azotes e ignominia, y no se borrará su afrenta.
34 Maana vivu humghadhibisha mtu; hatakuwa na huruma wakati wa kulipa kisasi chake.
Porque los celos excitan el furor del marido, y no tendrá compasión en el día de la venganza;
35 Ujapompa zawadi nyingi, hatakubali mbadala wa kusuruhishwa wala kulipwa.
no se aplacará por ninguna indemnización; no aceptará regalos, por grandes que sean.

< Mithali 6 >